Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda ameupongeza uongozi wa NMB kwa kubuni bidhaa bora na zinazoendana na watanzania wa kada zote akitolea mfano wa akaunti za Chap Chap.

Mh Pinda aliyasema hayo alipotembelea banda la NMB katika hoteli ya St. Gasper ya mkoani Dodoma ambapo PSPF wanafanya mkutano wao na NMB kama mdau mkubwa ameshiriki na kuweka mabanda ya huduma mbalimbali zikiwemo za NMB Wakala, NMB E- statement na Chap Chap Instant Account kwaajili ya washiriki wa mkutano huo.

Akaunti za Chap Chap ni za haraka na kumchukua mteja takriban dakika 10 tu kufungua akaunti na kupata ATM card papo hapo. Tekinolojia hii ni ya kipekee na inaweza kumfanya mtu akafungua akaunti yake popote alipo na kuanza kufaidi huduma mbalimbali kutoka NMB kupitia matawi Zaidi ya 170 na ATM mashine Zaidi ya 600 nchini kote.

Unangoja nini kuwa na akaunti ya NMB kama huduma zimerahisishwa kiasi hicho? NMB Karibu yako Zaidi.
Waziri Mkuu Mhe.Mizengo Pinda  akipata maelezo kutoka kwa  Afisa Mkuu wa kitengo cha biashara ya jumla wa NMB Ndugu Richard Makungwa juu ya huduma zaChap Chap Instant Acount na NMB Wakala. Huduma ya NMB Wakala humuwezesha mteja kutoa na kuweka fedha kupitia mawakala wa MaxMalipo waliotapakaa nchi nzima.
Maafisa wa NMB wakiwa kwenye Picha ya Pamoja na Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda na viongozi mbali mbali kutoka PSPF nje ya ukumbi wa Mkutano wa St Gasper ambapo Mkutano mkuu wa Nne wa wadau wa PSPF unafanyika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...