Na Teresia Mhagama

Balozi wa Marekani nchini, Mark Childress na Ujumbe wake, wamekutana na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachewene, katika makao makuu ya Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam.

Viongozi hao walikutana ili kuzungumzia masuala mbalimbali ikiwemo miradi ya umeme inayofadhiliwa na Mfuko wa Changamoto za Milenia (MCC), mradi mkubwa wa umeme unaofadhiliwa na nchi ya Marekani ujulikanao kama Umeme Afrika (Power Africa) pamoja na suala la kuwajengea uwezo watumishi wa Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake ili kuongeza uelewa na hivyo kuleta ufanisi wa kazi.
Waziri wa Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachewene (kulia) akishikana mkono na Balozi wa Marekani nchini, Mark Childress mara baada ya kumaliza mazungumzo yao jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachewene (kulia) akimsikiliza kwa makini Balozi wa Marekani nchini, Mark Childress (wa tatu kushoto) wakati Balozi huyo na ujumbe wake walipokutana Waziri wa Nishati na Madini jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Sharon Pauling, Naibu Mkurugenzi anayeshughughulikia Ukuaji wa Uchumi katika Shirika la Misaada la Marekani (USAID), (wa pili kushoto) na wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkaazi wa Mfuko wa Changamoto za Milenia nchini, Scott Alexander.
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachewene (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Marekani nchini, Mark Childress (wa tatu kushoto), wakati Balozi huyo na ujumbe wake walipokutana Waziri wa Nishati na Madini jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Sharon Pauling, Naibu Mkurugenzi anayeshughughulikia Ukuaji wa Uchumi katika Shirika la Misaada la Marekani (USAID), (wa kwanza kulia), Mkurugenzi Mkaazi wa Mfuko wa Changamoto za Milenia nchini, Scott Alexander (wa kwanza kushoto) na Merrica Dominick, Afisa Uchumi na Biashara katika Ubalozi wa Marekani nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...