Wakaazi wa wawili wa wilaya ya Hanang Mkoani Manyara kwa pamoja wamezawadiwa magari yao aina ya Toyota IST mara baada ya kuibuka washindi katika droo za promosheni ya Airtel yatosha Zaidi inayoendeshwa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel 
 Mpaka sasa jumla ya washindi 37 wameshapatikana kutoka katika mikoa mbalimbali ikiwa bado promosheni inaendelea na magari mengi bado yanasubiri washindi ili wakabithiwe akiongea wakati wa halfa ya kukabidhi magari kwa wateja wa Airtel Mkoani Manyara.
Meneja wa Airtel Kanda ya Kaskazini Bwana Brighton Majwala alisema: "Tunajisikia furaha kuendelea kupata washindi wa rika tofauti kutoka katika maeneo mbalimbali nchini, nasikia furaha kupata washindi kutoka katika kanda yangu.
"Hivyo naendelea kuwaasa watumiaji wa mtandao wa Airtel na wale ambao hawajajiunga kufanya hivyo na kupata nafasi ya kujishindia. promosheni bado inaendelea na magari bado yapo kinachotakiwa kufanya ni kununua na kujiunga na kifurushi chako cha Airtel yatosha zaidi na kupata nafasi ya kujishindia. nawapongeza sana washindi wetu wa leo na washindi wote ambao wameshapatikana mpaka sasa.
"Na nachoweza kusema ni kwamba Airtel tunajivunia kuwa sehemu ya kubadili maisha ya watanzania wengi hasa walio na kipato cha chini na kuwawezesha kufikia ndoto zao huku tukiendelea kurahisisha shughuli zao za kiuchumi na kijamii kupita huduma zetu na promosheni kama hizi. ni matumaini yetu kwa kupitia promosheni hii ya Airtel yatosha zaidi watanzania wengi wataguswa na kuboreshewa maisha yao". 
 Kwa upande wake Bwana Mohamed Ahmad Khamis ambaye ni mshindi wa gari aina ya Toyota IST alisema "Nimesikia furaha kubwa sana leo kupata ushindi huu mkubwa, kwangu hii imekuwa kama ndoto, mimi ni mtumiaji mzuri sana wa huduma za Airtel na ninazo line tatu za Airtel na hii moja leo imenipa ushindi. kwakweli nimeamini kabisa Airtel yatosha zaidi na inabadilisha maisha ya watanzania.
"Nimekuwa na ndoto za kumiliki gari lakini leo Airtel imeniwezesha kufikia malengo yangu na kunipa ushindi huu mkubwa na kuniwezesha kumiliki gari langu, nawashauri watanzania hasa wale wasioamini kuhusu promosheni hizi sasa waamini na kujua kwamba ni kweli promosheni hii na ni ya uhakika kwani mimi nimeshinda bila kuwa na taarifa yeyote. nawashukuru sana Airtel yatosha zaidi".
Naye mama Emiliana Tarmo Hhaway ambaye alizidiwa na furaha hadi kushindwa kuongea kwa lugha ya kiswahili alisema: "Nnamshukuru Mungu sana kwa kuniwezesha kushinda gari hili lakini pia nawashukuru sana Airtel kwa kuniwezesah kushinda. mimi nimenunua kifurushi cha Airtel yatosha cha shilingi mia tano na leo namiliki gari la mamilioni ya pesa ni jambo la kustaajabu sana. gari hili sasa litaniwezesha katika shughuli zangu za kilimo, kutoa mazao shambani kwenda sokoni, litanisaidia katika shughuli zangu za kijamii, kusaidia majirani hasa tukiwa na wagonjwa na nyingine nyingi. nasema asante sana kwa Airtel na kwa ushindi huu 
 Droo ya wiki ya 7 ya promosheni ya Airtel Yatosha inategemea kufanyika siku ya Alhamisi jioni ambapo washindi wengine 7 wa wiki hii watapatikana na kutangazwa

 Staff Sergeant wa wilaya ya Hanang Janet Mungolya akimkabithi funguo mshindi wa gari aina ya Toyota IST Bwn Mohamed Ahmed Khamisi mara baada  kuibuka mshindi wa droo ya wiki ya nne ya promosheni ya Airtel yatosha Zaidi.  Bi Emiliana ni mfanya biashara ndogo ndogo  na mkazi wa wilaya ya Hanang mkoani Manyara akishuhudia ni meneja mauzo wa Airtel kanda ya kaskazini bwana Brighton Majwala
 Staff Sergeant wa wilaya ya Hanang Janet Mungolya akimkabithi funguo mshindi wa gari aina ya Toyota IST Bi Emiliana Tarmo HHaway mara baada  kuibuka mshindi wa droo ya wiki ya tano ya promosheni ya Airtel yatosha Zaidi.  Bi Emiliana ni mkulima na mkazi wa wilaya ya Hanang mkoani Manyara akishuhudia ni meneja mauzo kanda ya kaskazini bwana Brighton Majwala
 Mshindi wa gari aina ya Toyota IST kupitia promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi bwana Mohamed Ahmed Khamisi akiwasha gari lake mara baada ya kukabithiwa gari yake katika halfa iliyofanyika katika uwanja wa mnada wa edasak wilaya ya Hanang mkoani Manyara

 Mshindi wa gari aina ya Toyota IST kupitia promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi Bi Emiliana Tarmo HHaway akifungua gari yake mara baada ya kukabidhiwa katika hafla iliyofanyika katika uwanja wa mnada wa edasak wilaya ya Hanang mkoani Manyara
Burudani katika hafla hiyo iliyofanyika katika uwanja wa mnada wa edasak wilaya ya Hanang mkoani Manyara

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...