Mwanasoka wa kike, Melanie Gines (kushoto) ambaye ni raia wa Hispania na bondia Omari Kimweri na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' wakiwa tayari kupanda ndege na kurudi kwao
Mwanasoka wa kike, Melanie Gines ambaye ni raia wa
Hispania (kushoto) akimkabidhi glove
kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'
katikati ni bondia Mtanzania
anayefanya kazi zake nchiniAustralia. Omari Kimweri ambaye aliongozana nchini
na mwanasoka huyo muda mfupi kabla awajapanda ndege kurudi kwao.
Na Mwandishi Wetu
BONDIA Mtanzania Omari Kimweri
anaefanya shughuli zake za mchezo wa masumbwi nchini Australia amempiga tafu ya
vifaa vya kufundishia kocha wa kimataifa wa mchechezo wa masumbwi nchini Rajabu
Mhamila 'Super D'
wakati wa zihara yake ya wiki mbili
ya kutembelea nyumbani kwa ajili ya kuwapa mabondia mbalimbali mbinu zitumiwazo
na mabondia wa nje
kabla ya hapo bondia huyo aliongea na
wadau mbalimbali wa masumbwi wakati wa mchezo wa ngumi za kulipwa kati ya Iddi
Bonge na Alphonce Mchumiatumbo mpambano uliofanyika katika ukumbi wa P.T.A
Sabasaba na kumvalisha mkata wa ubingwa bondia wa uzito wa juu Mchumiatumbo
baada ya kuibuka na ushindi wa K,O ya raundi ya kwanza
siku hiyo pia alimpiga tafu kocha
mkongwe wa mchezo wa masumbwi nchini Habibu Kinyogoli kwa kumkabidhi vifaa
vipya vya kufundishia mchezo wa masumbwiakizungumza baada ya kumkabidhi vifaa
kocha Super D alisema amekumbuka nyumbani kwa kuwa ndio alipo zaliwa na kitovu
chake kimezikiwa hapa nchini hivyo ataendelea kuwakumbuka zaidi kwa kuwawezesha
mabondia kucheza mara kwa mara pindi atakapoanzisha Kimweri Promotioon
itakayoshilikiana na Super D Boxing Coach And Promotion kwa kushilikiana
kuwapatia mabondia kupigana ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kujiongezea
kipato pamoja na kupandishe rekodi zao kwa mabondia chipukizi
nae kocha Super D
alishukulu kwa kukabidhiwa vifaa hivyo ambavyo vitamsaidia kuendelea kuinua
mabondia mbalimbali chipkizi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...