Philippe Coutinho (kushoto) baada ya kupiga bao kali wakati Liverpool walipotia pancha matairi ya gari la kutetea ubingwa la Manchester City katika mtanange wa Premier League uwanja wa Anfield jana.
Bwawa la maini walifungua dimba kwa bao la Jordan Henderson (picha ya chini) kabla ya Edin Dzeko kusawazisha kwa City. Lakini kiungo Mbrazil Coutinho alimaliza ubishi kwa bao la mita 25 lililowaacha kina Yaya Toure Midomo wazi.Matokeao hayo yanawaacha City wakiwa nyumba ya Chelsea kwa pointo tano, huku Liverpool tukipanda hadi nafasi ya tano. Bwawa la Maini Oye!
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...