Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi kwa kupeleka zege kwenye eneo husika wakati wa ujenzi wa daraja la Kisongo,ambalo lilikuwa kero kubwa kwa wananchi kutokana na barabara ya eneo hilo kulika na mmomonyoko wa udongo.
Ujenzi wa daraja la Kisongo ukiendelea kwa kasi,ambapo pia Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana alikagua na kushiriki ujenzi wake.
Baadhi ya wananchi wa Kisongo wakipita juu ya barabara ambayo imeanza kuathirika na mmomonyoko wa udongo.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kuweka zege wakati wa ujenzi wa kituo cha afya cha Manyire,ujenzi wa kituo hicho unatarajia kuisha mwaka huu ambapo kiasi cha fedha zaidi ya shilingi milioni 500 zitakuwa zimetumika kukamilisha ujenzi huo. 
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ngaramtoni ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa CCM ya sasa haitofanya makosa, na kuwahakikishia kila atakayefanya makosa itabidi aubebe msalaba wake. 
 Mbunge wa jimbo la Arumeru Magharibi Ndugu Goodluck Ole Medeye akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nduruma ambao walikuwa na malalamiko juu ya mradi wa maji wa Nduruma kuonekana kupelekwa mashambani badala ya maeneo wanayoishi wananchi.Ndugu Kinana wa pili kushoto alikuwepo kusikiliza malalamiko hayo na kuwapatia majibu.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ngaramtoni ambapo alitoa sababu mbali mbali za dalili za kufa kwa upinzani nchini.
Mhariri wa Gazeti la Jambo Leo,Said Mwishehe akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana kabla ya mkutano wa hadhara kufanyika ndani ya jimbo la Arumeru Magharibi,pichani shoto ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisikiliza.Ndugu Kinana yupo kwenye ziara ya kikazi ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.


PICHA NA MICHUZI JR-ARUMERU MAGHARIBI ARUSHA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...