Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe (kushoto), akimkabidhi zawadi ya kumbukumbu Mwakilishi Mkuu wa zamani wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) Yasunori Onishi, ofisini kwake jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi nchini.Mwakilishi huyo ameishukuru Wizara ya Ujenzi kwa ushirikiano aliopata katika kipindi chote alichohudumu nchini.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe (kushoto), akimkabidhi zawadi Mwakilishi Mkuu mpya wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) Toshio Nagase (kulia) Ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe akifurahi jambo na Ujumbe kutoka wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) wakati ugeni huo ulipotembelea ofisini kwake kwa lengo la kutoa pongezi za JICA kwa Wizara ya Ujenzi kutokana na utekelezaji mzuri wa miundombinu ya barabara.Picha na Habari kwa Hisani ya Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Ujenzi.

---
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe amelipongeza Shirika la Misaada ya Maendeleo la Japan (JICA) kwa ufadhili wa miradi mingi ya ujenzi wa miundombinu ya barabara iliyokamilika na inayoendelea nchini.

Eng. Iyombe ametoa pongezi hizo leo jijini Dar es Salaam wakati akiagana na Mwakilishi Mkuu wa JICA nchini Bw. Yasunori Onishi, ambae amemaliza muda wake na kumpisha Mwakilishi Mkuu mwingine Bw. Toshio Nagase.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...