Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa amebeba maji kwenye madumu aliposhiriki umwagiliaji maji katika shamba la nyanya la vijana wajasiriamali wa CCM katika Kijiji cha Nkulabi, Kata ya Mpunguzi, Jimbo la Dodoma Mjini leo wakati wa ziara yake,Kinana yupo mkoani Dodoma kwa ziara ya siku tisa ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi, kuimarisha uhai wa chama na kusikiliza kero za wananchi pamoja na kuzitafutia ufumbuzi.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akimwagilia maji zao la nyanya la vijana wajasiriamali wa CCM katika Kijiji cha Nkulabi, Mpunguzi, Dodoma. Kinana aliwapongeza vijana hao wanne kwa kuamua kuanzisha shamba hilo ambalo mazao yake yanawasaidia kujikimu kimaisha.Kinana aliwataka vijana wengine kuiga mfano huo.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akihutubia katika mkutano wa hadhara mjini Dodoma, ambapo ametoa ushauri kwa Katibu Mkuu Kiongozi, kuwasimamisha mara moja watumishi wanaotajwa kwenye sakata la Escrow kama CCM ilivyowasimamisha viongozi watatu waliotajwa kwenye sakata hilo.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Dodoma mjini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya  Barafu,Nape aliwaambia wakazi hao kuwa makini na wapinzani kwani wamekuwa wakihangahika na fedha za wafadhili ambazo hawaitakii mema nchi yetu.
 Pichani ni baadhi ya Wafuasi wa chama cha CCM na wananchi wakishangilia jambo kwenye mkutano huo. 

PICHA NA MICHUZI JR-DODOMA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Kinana sasa KILIMO KWANZA inayojumuisha maji ya mifereji, mabwawa, mbolea, matrekta, masoko ya uhakika, viwanda vya kusindika mazao kuongeza thamani kwa mkulima lini yatatimizwa?

    Maana hizi harakati za kutumia misuli zitakuumiza Mzee wetu tafuta namna KILIMO KWANZA kilete Matokeo Makubwa SASA.

    ReplyDelete
  2. Mh kinana unafanya kazi Nzuri sana upande wa chama ila unaangushwa upande wa serikali kwa kweli.

    ReplyDelete
  3. Usanii ni kazi vilevile

    ReplyDelete
  4. Watumie Drip Irrigation. Hata vijana hao wakibeba maji mabegani Kilimo watakiona kuwa ni adhabu.

    ReplyDelete
  5. Teknolojia bado ni ndoto Tanzania. Kwa kubeba maji namna hii utalima hekari ngapi? au tunazungumzia kulima chakula cha familia yapo peke yake??

    ReplyDelete
  6. Kinana akimaliza hizi hekaheka lazima achukue likizo ya miaka miwili apumzishe mwili.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...