Picha juu na chini ni mwandishi wa habari za michezo wa gazeti la Bingwa, Dimba na
Mtanzania kutoka Kampuni ya New Habari 2006 Ltd, Sharifa Mmasi pichani
akisoma kitabu cha Dira na Tumaini Jipya Handeni kilichoandikwa na Kambi
Mbwana, ambaye ni Mratibu Mkuu wa Tamasha la Handeni Kwetu
linalofanyika kila mwisho wa mwaka wilayani Handeni, mkoani Tanga.
Na Mwandishi Wetu,
Dar es Salaam
Kitabu hicho kimeelezea kero na changamoto mbalimbali za
wananchi wa Handeni, kama vile shida ya maji, elimu na migogoro ya ardhi kwa
ajili ya kushirikisha mawazo ya viongozi wa serikali, wadau na wananchi ili kukabiliana
na tatizo hilo wilayani humo na mikoa ya jirani ambapo changamoto hizo
zinashabihiana kwa kiasi kikubwa.
Kwa habari kamili BOFYA HAPA
Kwa habari kamili BOFYA HAPA
Nakupongeza kwa kuandika kitabu kuhusu habari ya kwenu na changamoto zilizopo. Kitabu hiki kitumike kuweka mipango mizuri y kutatua kero hizo.
ReplyDelete