Mwandishi Wetu

Wakati bondia Mohamed Matumla Jr akiwa katika mazoezi ya mwisho mwisho kumkabili Wang Xin Hua wa China, wenzake Thomas Mashali na Karama Nyilawila wametoleana uvivu huku kila mmoja akijigamba kutwaa ubingwa watakapozichapa Machi 27 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.

Matumla Jr atazichapa na Hua pambano la super bantam la ubingwa wa dunia wa (WBF World Eliminate) pambano maalumu kwa mabondia hao la kutafuta tiketi ya kucheza pambano la utangulizi kwenye lile la nguli wa masumbwi duniani, Manny Pacquiao na Floyd Mayweather la Mei 2. 

Kama Matumla atampiga Hua kwenye pambano lao la Machi 27 na kuonyesha kiwango kizuri atapata nafasi ya kucheza pambano la utangulizi kuwasindikiza nguli hao wa masumbwi duniani watakapovaana Mei 2 jijini Las Vegas.

Akizungumza katika mazoezi yake yanayoendelea kwenye gym ya Oil Com, Keko jijini Dar es Salaam chini ya kocha wake ambaye ni baba yake mzazi, Rashid 'Snake Man' Matumla, bondia huyo alisema hataki kupoteza nafasi ya kucheza kwenye pambano la Mayweather na Pacquiao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...