Mwandishi Wetu
Wakati bondia Mohamed Matumla Jr akiwa katika mazoezi ya mwisho mwisho
kumkabili Wang Xin Hua wa China, wenzake Thomas Mashali na Karama
Nyilawila wametoleana uvivu huku kila mmoja akijigamba kutwaa ubingwa
watakapozichapa Machi 27 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar
es Salaam.
Matumla Jr atazichapa na Hua pambano la super bantam la ubingwa wa
dunia wa (WBF World Eliminate) pambano maalumu kwa mabondia hao la
kutafuta tiketi ya kucheza pambano la utangulizi kwenye lile la nguli
wa masumbwi duniani, Manny Pacquiao na Floyd Mayweather la Mei 2.
Kama Matumla atampiga Hua kwenye pambano lao la Machi 27 na kuonyesha
kiwango kizuri atapata nafasi ya kucheza pambano la utangulizi
kuwasindikiza nguli hao wa masumbwi duniani watakapovaana Mei 2 jijini
Las Vegas.
Akizungumza katika mazoezi yake yanayoendelea kwenye gym ya Oil Com,
Keko jijini Dar es Salaam chini ya kocha wake ambaye ni baba yake
mzazi, Rashid 'Snake Man' Matumla, bondia huyo alisema hataki kupoteza
nafasi ya kucheza kwenye pambano la Mayweather na Pacquiao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...