Kumbukizi maalum ya tarehe 20 Machi 2015 ya wanafunzi watano wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM) waliopoteza maisha katika ajali ya barabarani imetukumbusha msiba mkubwa wa watu 50 katika ajali moja ya basi na lori ya tarehe 11 Machi 2015.

Wakati tukiendelea kuwaombea marehemu na majeruhi na kutoa pole kwa wafiwa na wahanga wakati umefika sasa tutangaze #AjaliBarabaraniJangalaTaifa tuwajibike kuzipunguza.

Kumbukizi katika ukumbi wa Nkurumah ilihusisha ibada, nyimbo maalum na kusomwa kwa wasifu wa wanafunzi walioaga dunia wakiwa wadogo familia zao na taifa likiwahitaji na hatimaye salamu kutoka makundi mbalimbali.

Niliguswa na salamu za Chuo cha Fani za Jamii zilizosomwa na Mkuu wa Chuo cha Fani za Jamii aliyeeleza kwamba mabasi sasa yanaua kuliko magonjwa mengi.

Alipendekeza utafiti ufanyike UDSM kuchangia kupunguza hali hiyo kwa kuzingatia kwamba Chuo Kikuu hicho kina fani mbalimbali (multi disciplinary).

Alieleza kwamba kwa upande wa uhandisi waangalie iwapo teknolojia ya mabasi yenye spidi inawiana na barabara zetu kuu ambazo nyingi ni za njia moja. Huku fani ya jamii iangalie masuala ya maadili kufanya madereva wa mabasi kujifunza kwamba wanabeba binadamu sio wanyama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ile ajali inauma sana mpaka leo na kesho. Usiambiwe na usiombe ukutwe na janga kama hilo awe ndugu yako au mzazi or rafiki hata mtu yeyote. Jamani ile ajali inaniuma roho. Sielewi shetani gani asiyesikia sala na maombi ya watu anaangamiza watu kiasi hiki. Ila Mungu anaona na anajibu maombi tuzidi kusali kuombea usalama wa abiria wetu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...