Na   Bashir  Yakub.

Jumatatu  ya  wiki  hii nilianza  na  makala  iitwayo   je  umeachishwa  kazi  au we  ni  mfanyakazi,  zijue  haki  zako. Nilizungumzia  masuala  kadhaa  yahusuyo  haki  za  mfanyakazi. Naligusia  kuhusu  aina  za  mkataba wa ajira, muda wa mkataba  wa ajira,  sehemu  ya  kufanyia  kazi, kipindi  cha  mpito katika  kazi (probation period) na mengine  mengi kuhusu  ajira. Nilisema  na  leo  tena  nasisitiza  kuwa  ili  upate  ujira  unaostahili   ikiwa  ni  pamoja  na  mafao kwa  kiwango  kinachotakiwa baada  ya kumalizika  kwa  ajira  yako  huna  budi kuwa  unajua  haki  zako.  Usisubiri  mwajiri  akwambie  nini  unastahili  isipokuwa  wewe  ndio  umwambie  mwajiri  nini  unastahili. 

 Mwajiri  hawezi  kukufundisha  haki  zako  kwakuwa  utazitumia kumnyima  amani. Nilisema  pia  kuwa  yawezekana unachopata  na  ukaona  kingi  sicho  unachostahili  kupata  usipokuwa tu  hujui. Kwahiyo  niseme  tu  kwamba  ni  muhinmu  mfanyakazi  kujishugulisha  kujua  haki zako  japo  chache. Leo  tunaangalia  tena  baadhi  ya  haki  nyingine  lakini  kabla  ya  hapo  ni  ushauri. 

USHAURI  KWA  WAFANYAKAZI.

Haki  za  mfanyakazi  ninazoeleza  hapa  yawezekana  wakati  ukiwa  kazini  unaogopa  kuzidai  kutokana  na  woga  wa  kuonekana  umekuwa mjuaji  na  hivyo kukaribisha uwezekano wa  kupoteza  ajira. Pia  waweza kuwa uliacha  kuzidai  kwakuwa  huzijui. Kama  moja kati  ya  haya   limekutokea  basi  ushauri wangu  ni  kuwa haki  hizi zote  waweza  kuzidai  baada  ya  kuwa  umeachishwa  kazi  au wakati  wa  kustaafu  kwani  sheria  inaruhusu. Kama  hukupewa overtime,ulifanyishwa  kazi  muda  wa sikukuu, hukupewa  likizo kama  inavyostahili  na  yote  nitakayoeleza  hapa  chini basi  baada  ya  kazi  kuisha  waweza  kudai  fidia  yake.

1.  HAKI  YA  KUJUA  MASAA  YA  KAZI.

Mfanyakazi  hafanyi  kazi  muda  wote. Akifanya kazi  muda  wote  basi  uwe  ni uamuzi binafsi  lakini  lisiwe  ni agizo  la  mwajiri. Kazi  ina  muda  wake  na  hii  ni  kwasababu ili  mwanadamu  aishi  pia anahitaji kuhusika  katika  mambo  mengine  ya  kimaisha  nje  ya  kazi. Kutokana  na  hilo  ni  lazima  mkataba  wa ajira  uoneshe masaa  anayotakiwa  mtu  kufanya  kazi.  Kama  ni  masaa  12, masaa  8, masaa 9 yajulikane. Na  ni hayo hayo  tu  mfanyakazi  anayotakiwa  kufanyia  kazi.  Faida  ya  kuainisha  masaa  ya  kazi  ni kuwa  humsaidia  mfanyakazi  kupata  malipo  ya  ziada  iwapo   masaaa  yaliyoainishwa  yamepita. Hii wengi  wanaijua  huitwa  overtime. Overtime  ni  haki  ya  msingi  ya  mfanyakazi  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...