NA  BASHIR  YAKUB

Makuzi ya biashara hasa biashara za kimataifa yameleteza utitiri wa makampuni. Karibia kila biashara kubwa au ya kati  kwa sasa  hufanywa na makampuni. Baadhi ya ndani na mengine  ya nje. 

 Hatua hii njema kwa kiasi  fulani imeongeza  ajira  japo ajira zenyewe hazina vigezo vya kuitwa ajira. Yatosha ziitwe kazi tu. Ajira hizi ambazo nyingi  ni za umanamba zimekuwa  zikifanywa na wazawa.  Upande mmoja zimekuwa neema na upande mwingine zimekuwa laana. 

Ni neema kwakuwa baadhi  wanaweza kuishi japo  kwa pato la mlo tu na kusiwe na akiba yoyote  lakini  pia zimekuwa laana kwakuwa  ukihadithiwa baadhi ya mambo yanayoendelea huko waweza toa chozi.

Sio pote ila yapo maeneo yaliyoshindikana kama viwandani, migodini, miradi ya barabara na kwingineko waliko wawekezaji hasa wa kigeni. Hili ndilo limenituma kuandaa makala haya ili basi wenye  fursa wasome na waelewe na wenye kutaka msaada waweza kuwasiliana nami na kuona la kufanya.

Nianze hivi, kampuni kwa mujibu wa sheria ni mtu( legal person). Kuna tofauti kubwa kati ya kampuni na mmiliki wake. Kisheria kampuni  ikifanya kosa  yatakiwa ishitakiwe kampuni na sio  wamiliki au mfanyakazi kama mameneja, mkurugenzi n.k. 

Nimewaona wengi  hasa vijana ambao  huyadai makampuni haki zao hufungua kesi wakiwashitaki  wamiliki au mabosi wao. Hili ni kosa kubwa na wengi wao huwa wanashindwa zile kesi  na badala yake  kuanza kulalamikia mfumo wa nchi , mahakama au viongozi na hata chama tawala.

Ndugu hili halikusaidii. Hili sio  la serikali wala rais wala nani ni suala ka kisheria. Kampuni yako imekukosea unataka kudai fidia umemshtaki mmilki au viongozi badala ya kampuni, ni lazima utashindwa kesi  usimtafute mchawi wala kulalama kwa tuhuma za rushwa. Unapokosea taratibu  sheria haina huruma inakata. Upo msemo usemao (  A law is a merciless sword) yaani sheria ni upanga usio na huruma unamkata yeyote anayeuchezea. Kampuni  kama kampuni inao uwezo wa kushtaki kwa jina lake na kushtakiwa kwa jina  lake,namna gani tutaona hapo chini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...