Na Bashir
Yakub.
Suala la matunzo ya watoto/mtoto lim ekuwa
ni suala ambalo wasomaji
wengi wamekuwa wakiniuliza sana. Wengi wao
wanaouliza ni wale
ambao wamezaa nje
ya ndoa na
hivyo kuna utata
wa matunzo ya
watoto na wale
ambao wamekuwa wana ndoa lakini
sasa tayari wametengana
aidha kwa talaka
au bila talaka. Niseme tu
kwa ufupi kuwa suala
la matunzo ya watoto
linajumuisha mambo mengi nami
nitaeleza baadhi
tu.
1.HUWEZI KUMLAZIMISHA
MTOA MATUNZO KUTOA
AMBACHO HANA.
Kumekuwepo na tabia
ya wazazi hasa
upande wa wazazi
wa kike kuwalazimisha wanaume
ambao wamezaa nao
na kutengana nao
kutoa matunzo ya
watoto kwa kiwango
cha juu kabisa
ambacho pengine kinazidi
hata kipato cha
mtoaji. Hili si sawa.
Ni kweli sheria inamlazimisha
mwanaume kutoa matunzo
ya mtoto lakini
haimlazimishi kutoa kuliko
anachopata. Sheria haiseme kwakuwa
mwanamke anaishi na
mtoto wa mtu
basi mwanaume ndio sasa afanywe
kitega uchumi. Inafikia
hatua mwanamke hafanyi
kazi yoyote isipokuwa
anategemea ile pesa
ya matunzo ya mtoto
ndio iwe kila
kitu katika maisha
yake.
Hii ndio sababu
hata akipewa kiasi
kinachotosha haoni kama
kinatosha kwakuwa kinakuwa na njia nyingi
kama saluni, nguo za kuvaa, pesa
ya upatu, michango ya
harusi na kitchen party
na kila kitu kinachohusu maisha
yake binafsi. Ieleweke wazi
kuwa kwa mujibu
wa sheria pesa
ya matunzo ya mtoto haihusiki
na haya. Pesa
ya matunzo ya
mtoto ni pesa
ya matunzo ya mtoto kama neno
lenyewe lilivyo na linavyojieleza
si vinginevyo.
2.INARUHUSIWA KUKATAA
IKIWA UNALAZIMISHWA KUTOA
MATUNZO YANAYOZIDI UWEZO WAKO.
Ikiwa mwanaume analazimishwa
kutoa kuliko kipato
chake basi anaruhusiwa
kukataa hata kama
amri hiyo imetolewa
na mahakama. Wengine huandikishana
polisi lakini bado
haibadili maana kwakuwa
mtu anatakiwa kutoa
kulingana na uwezo wake
au kipato chake. Wapo
wazazi hasa wa kike
ambao huwalazimisha wanaume
kutoa matunzo ya kuwasomesha
watoto international schools
wakati kipato cha
mwanume ni shule
ya kata. Sheria inachokataza
ni kukataa kabisa
kutoa matunzo ya mtoto
lakini haimlazimishi mtu
kutoa kilichomzidi. Au
wengine hulazimisha kuwekewa
mpaka wafanykazi wa ndani(
house girl) wakati kipato
cha mwanaume hakiruhusu
jambo hilo.
Huu nao ni
unayanyasaji kwa upande
wa wanaume na
haukubaliwi na sheria. La
msingi ni kuwa
iwapo utalazimishwa kutoa
kuliko uwezo wako
we kataa. Na
kama uamuzi huo
umetolewa na mahakama
basi kataa kwa kukata
rufaa kupinga kabisa
jambo hilo. Sheria inaposema
matunzo ya watoto
haisemi kuwa watu
watoe kuliko uwezo wao hapana.
Sheria ni haki
na haki huzingatia
ukweli na hali
halisi ya jambo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...