Makamu Mwenyekiti wa Kampuni ya Huawei,Ken Hu akizungumza
katika Mkutano wa Dunia wa masuala ya simu (MWC) uliofanyika jijini
Barcelona nchini Hispania mwishoni mwa wiki iliyopita,uliokuwa ukijadili
teknolojia ya simu za mkononi (5G).
Kizazi
cha tano cha teknolojia ya simu za mkononi (5G) kinategemewa kuwa nguzo
muhimu sana ya miundo mbinu katika ulimwengu ujao wa teknolojia. Hayo
yamesemwa na Bwana Ken Hu, Makamu mwenyekiti wa Kampuni ya Huawei ambaye
kwa kupokezana yeye ndiye Mkurugenzi Mtendaji kwa sasa.
Akizungumza katika Mkutano wa Dunia wa masuala ya simu (MWC) uliofanyika jijini Barcelona nchini Hispania mwishoni mwa wiki iliyopita, Mr, Hu alisisitiza kwamba maono ya kuwa na teknolojia ya 5G yatafanikiwa kupitia ushirikiano wa sekta mbalimbali, ubunifu makini katika teknolojia na mageuzi katika mikakati ya kibiashara.
“Msukumo mkubwa wa kuwa na teknolojia ya 5G unahusisha mahitaji ya kumwezesha mtumiaji kupata urahisi kutumia, uwezekano wa vifaa vingi zaidi kutumia Internet katika maisha ya kila siku, na mahitaji ya kuwa na watoa huduma wanaozingatia sekta maalum pekee katika mapinduzi ya viwanda siku zijazo” Alisema Bwana Hu.
Akizungumza katika Mkutano wa Dunia wa masuala ya simu (MWC) uliofanyika jijini Barcelona nchini Hispania mwishoni mwa wiki iliyopita, Mr, Hu alisisitiza kwamba maono ya kuwa na teknolojia ya 5G yatafanikiwa kupitia ushirikiano wa sekta mbalimbali, ubunifu makini katika teknolojia na mageuzi katika mikakati ya kibiashara.
“Msukumo mkubwa wa kuwa na teknolojia ya 5G unahusisha mahitaji ya kumwezesha mtumiaji kupata urahisi kutumia, uwezekano wa vifaa vingi zaidi kutumia Internet katika maisha ya kila siku, na mahitaji ya kuwa na watoa huduma wanaozingatia sekta maalum pekee katika mapinduzi ya viwanda siku zijazo” Alisema Bwana Hu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...