Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Makamu wa Rais wa Shirika la Simu Vitnam (VIETTEL) Hoang Son, wakati Makamu huyo alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Machi 9, 2015 kwa mazungumzo akiwa ameongozana na ujumbe wake.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Makamu wa Rais wa Shirika la Simu Vitnam (VIETTEL) Hoang Son (wa pili kushoto kwake) na ujumbe wake Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Viettel Global, Tao Duc Thang, Mshauri wa Viettel Tanzania, Francis Mndolwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Nguyen Thanh Quang, wakati Makamu huyo alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Machi 9, 2015.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa Kampuni ya Viettel, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika leo Ofisini kwake Ikulu. Picha na OMR.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...