Ofisa Mtendaji Masoko wa EATV, Brendansia Kileo (kulia)
akifafanua jambo mbele ya wandishi (hawapo pichani), kushoto kwake ni Digital
&Branding Manager wa 361 degree, Hurbert Kissas na kulia ni Meneja wa chapa
wa vinywaji vikali wa Serengeti Breweries Limited, Shomari Shija.
Maonyesho ya siku mbili ya Harusi Tanzania maarufu kama
‘Harusi Trade Fair 2015’, yanayotarajiwa kufanyika Machi 13-14 mwaka huu katika
ukumbi wa Danken House, uliopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Wakiongea na wandishi wa habari mapema jana Machi 2, wakati wa kutambulisha
wadhaamini wakuu wa mwaka huu ambao ni kampuni ya Bia ya Serengeti, kupitia kwa
vinywaji vya Baileys ‘Cream with Spirit’ na Johnnie Walker ‘Gold Label’,
wandaaji wa maonyesho hayo kampuni ya 361 degree, kupitia kwa Meneja biashara
na maendeleo, Hamis Omary alisema tayari
maandalizi hayo yamepamba moto huku washiriki zaidi ya 50, wakitarajiwa
kushiriki.
“mwaka huu ni wa sita kwa maonyesho
haya. Hivyo tunajivunia
mafanikio mbalimbali. Tunashukuru wadhamini wetu kampuni ya bia ya
Serengeti kwa kujitokeza kudhamini mwaka huu ni faraja kwetu” alisema
Hamis Omary.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...