Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akizungumza na mmoja wa wanufaika wa mkopo kwa akina mama na vijana uliotolewa kwenye Kata zote za Manispaa hiyo, Victoria Mboweto alipotembelea mradi wake wa duka la nguo, Kigogo Mbuyumi, Dar es Salaam juzi. Manispaa hiyo imetenga kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajili ya kukopesha vikundi vya akina mama na vijana katika Kata zake.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akizungumza na mmoja wa wanufaika wa mkopo kwa akina mama na vijana uliotolewa na Manispaa hiyo kwa Kata zote, Semeni Mahita ambaye ana mradi wa kuuza vitafunwa na mbogamboga sokoni alipotembelea mradi wake Kigogo Mbuyumi, Dar es Salaam juzi. Manispaa hiyo imetenga kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajili ya kukopesha vikundi vya akina mama na vijana katika Kata zake. Wapili kushoto ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana wa Manispaa hiyo, Mwajuma Magwiza.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akizungumza na mmoja wa wanufaika wa mkopo kwa akina mama na vijana uliotolewa na Manispaa hiyo kwa Kata zote, Semeni Mahita ambaye ana mradi wa kuuza vitafunwa na mbogamboga sokoni alipotembelea mradi wake Kigogo Mbuyumi, Dar es Salaam juzi. Manispaa hiyo imetenga kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajili ya kukopesha vikundi vya akina mama na vijana katika Kata zake. Kushoto ni mmoja wa wateja wa mwanamama huyo.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (kushoto) akikagua mradi wa kuchakata vikoi na mashuka wa mmoja wa wanufaika wa fedha za mkopo za akinamama na vijana wa Manispaa hiyo, Thresia Mazwazwa (kulia kwake) alipotembelea mradi wake, Sinza, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Manispaa hiyo imetenga kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajili ya kukopesha vikundi vya akina mama na vijana katika Kata zake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...