Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, akifungua Mkutano wa 59 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu Hadhi ya Wanawake ( CSW), Mkutano huu wa wiki mbili ulioanza siku ya jumatatu, unafanyika ikiwa ni miaka 20 tangu kufanyika kwa mkutano wa kihistoria wa wanawake uliofanyika Beijing, China mwaka 1995. Mkutano huo uliokuwa chini ya Ukatibu Mkuu wa Dr. Gertrude Mongella, uliweka misingi mbalimbali iliyolenga katika kusimamia na kutetea haki mbalimbali za mwanamke zikiwamo za usawa wa kijinsia na uwezeshwaji.
Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akiwa na sehemu ya Ujumbe wa Tanzania unaoshiriki Mkutano wa 59 wa Kamisheni kuhusu Hadhi ya Wanawake ulioanza jana jumatatu hapa Umoja wa Mataifa.
Sehemu wa washiriki wa mkutano wa 59 wa Kamisheni kuhusu Hadhi ya Wanawake wakifuatili hotuba za ufunguzi zilizotolewa na viongozi mbalimbali akiwamo Katibu Mkuu Ban Ki Moon na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Bw. Sam Kutessa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...