Inocent Melleck akizungumza na baadhi ya wananchi waliojitokeza kumchangia fedha kwa ajili ya kuchukulia fomu za kuwania Ubunge katika jimbo la Vunjo.
Innocent Melleck akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wananchi hao waliojitokeza kumchangi fedha kwa ajili ya kugombea Ubunge katika jimbo la Vunjo.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
MBUNGE wa jimbo la Vunjo,Agustino Mrema(TLP) ameendelea kupata
upinzani katika Jimbo lake baada ya baadhi ya wananchi kujitokeza
hadharani na kumchangia pesa,Innocent Melleck Shirima kwa lengo la kumchukulia
fomu wakati wa kugombea nafasi ya Ubunge kwa tiketi ya Chama cha
Mapinduzi.
Tayari joto la uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba mwaka huu limeanza
kushika kasi katika jimbo hilo baada ya Mwenyekiti wa Chama cha NCCR
–Mageuzi,James Mbatia kuombwa na wananchi wa jimbo hilo kugombea
nafasi ya Ubunge.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...