Dr. Natalius Kapilima wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya akimpima shinikizo la damu Bw. Exadius Nthono wa Lesotho katika mkutano wa mwaka wa wahasibu waandamizi unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere ambapo NHIF inatoa huduma za upimaji afya bure. 

Na Catherine Kameka

WADAU wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wameuomba Mfuko huo kuendeleza programu za upimaji wa afya bure ili kuwasaidia wanachama wake na wananchi kwa ujumla kujua hali za afya zao lakini pia kuepekana na maradhi yasiyoambukiza.

Hayo wameyasema Dar es Salaam jana katika mkutano wa Wahasibu Waandamizi wa nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika, unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu J.K.Nyerere ambapo NHIF ilishiriki kwa kuwa na banda la elimu kwa umma na upimaji wa afya bure uliokwenda sambamba na utoaji wa elimu ya namna ya kujikinga na maradhi yasiyoambukiza kama moyo na mengine.

Pamoja na ombi hilo, NHIF imekuwa ikiendesha upimaji katika maeneo mbalimbali ya nchi kwa lengo la kuwasaidia wananchi kufahamu afya zao lakini pia kuwapa ushauri wa namna ya kujikinga na maradhi hayo ambayo yamekuwa yakiongezeka kwa kasi na matibabu yake ni ya ghari.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...