Katika mwendelezo wa kuwa karibu na wateja wake benki ya NMB imezindua mtandao utakaowaunganisha wateja wake wakubwa ‘Executive Network’ kwa jiji la mbeya ikiwa na lengo la kuwafanya kufurahia zaidi huduma za kibenki kutoka NMB. 
 Uzinduzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mbeya na kuwakutanisha wafanyabiashara zaidi ya 100 kutoka vitongoji mbali mbali ikiwemo Kyela, Mbozi,Tunduma, Mwanjelwa, Mbalizi Road na Usongwe waliopata fursa ya kuwa kwenye mtandao wa wafanya bishara wa NMB. 
 Mtandao huu unaounganisha wateja wakubwa wa NMB vile vile umezinduliwa katika mikoa mbalimbali ikiwemo; Arusha, Mwanza, Dar es Salaam na Mbeya ikiwa ya nne.
Afisa Mkuu wa Wateja  Wakubwa na Serikali wa NMB - Richard Makungwa(pili kulia) pamoja na Given Ngajilo wa kampuni ta Tunhimbaghe Traders Ltd (mteja).Wakifungua pazia kuashiria uzinduzi rasmi wa NMB Executive Network jijini mbeya huku wakishuhudia ni Mkuu wa kitengo cha wateja wakubwa wa NMB - Filbert Mponzi (kulia) na menejaa wa NMB Nyanda za juu- Lucrecia Mkarie
Maafisa wa NMB wakifurahi pamoja na mteja wao baada ya uzinduzi rassmi wa mtandao wa ‘NMB Executive Network’
Sehemu ya wateja wakubwa wa NMB walioalikwa katika uzinduzi huo.
Mmoja wa wateja wakubwa wa NMB akiomba ufafanuzi juu ya huduma zitolewazo na benki hiyo  wakati wa hafla iliyowakutanisha wateja wakubwa wa benki ya NMB.
Meneja Maendeleo ya Biashara wa NMB, Masato Wasira(kushoto) na Mtaalam Mwandamizi wa bidhaa za hazina kwa wateja wakubwa ,Ronald Kato  wakiwa pamoja na wateja wa NMB kutoka kampuni ya Sunshine Mining ya Chunya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...