Vurugu kubwa zinaripotiwa kutokea leo maeneo ya Olasiti jijini Arusha baaada ya habari ambazo bado kuthibitishwa rasmi zimeanza kufuatia mtu mmoja kukuta mfanyakazi wake wa kike akiwa  amelala  na anayedaiwa kuwa mpenzi wake ndani ya nyumba anayofanyia kazi. 
Inasemekana baba mwenye nyumba alikasirika sana kwa kitendo hicho na akampiga huyo kijan hadi akafa. Ndipo marafiki wa huyo anayedaiwa kuuwawa wakakusanyika nyumbani hapo na kuchoma moto nyumba na magari mawili kabla askari wa kutuliza ghasia kufika na kupambana nao kwa masaa kadhaa. Habari kamili na rasmi itawajia mara baada ya kupatikana
Nyumba hiyo ikiungua moto
Sehemu ya nyumba hiyo na gari 
Moja ya magari yaliyochomwa moto
Gari lingine lililochomwa moto
Majirani na wapita njia wakiangalia nje ya nyumba hiyo.
Picha na Gadiola Emmanul wa Tanzania Bloggers Network

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Watu wengine ni sheeda,unaua kwa kumfumania HG? Ameshindwa busara hata na Kingwendu!.aliyemsamehe mgoni wake..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...