Na. Johary Kachwamba-MAELEZO, DODOMA

SERIKALI kupitia Mamlaka ya Maeneo ya EPZ pamoja na Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) imeweka matayarisho na utaratibu wa kuvutia wawekezaji eneo la Tanga.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Janet Mbene alipokuwa akijibu swali la msingi la Mhe. Omari Nundu, Mbunge wa Tanga Mjini.

“tayari Mamlaka ya EPZ imetenga hekta 1,363 katika eneo la Neema mkoani Tanga kwaajili ya ujenzi wa viwanda na uthamini wa mali umekamilika” alisema Mhe. Mbene

Aidha Mhe. Alisema NDC ina eneo la hekta 50 huko Kange Mkoani Tanga ambalo maandalizi ya kuliweka tayari kwaajili ya kuvutia uwekezaji yanaendelea.

Juhudi za kuvutia uwekezaji ili kuanzishwa viwanda vipya zimefanyika pia ambapo kuna viwanda vingi vimeanzishwa ikiwa ni pamoja na Kiwanda cha Maweni cha Saruji, Athi River cha Chokaa, Neelkanth cha chokaa, Tanga Pharmaceutical and Plastics LTd, Peepe Tanzania Ltd, Pemba Flour Mill na vinginevyo. 

“kiwanda cha Saruji cha Tanga na Tanga Fresh ni baadhi ya viwanda vilivyoboreshwa mkoani Tanga ambavyo vinafanya kazi na kuongeza uzalishaji. Kiwanda cha Tanga Dairies Ltd, Tanga kilifufuliwa na sasa kinafanya kazi” alisema Mhe. Mbene

 “Serikali imetambua kuwa tatizo la kiwanda cha mbao linatokana na gharama kubwa ya kupata malighafi kutoka Mufindi, Iringa hadi Tanga. Kutokamilika kwa makabidhiano baina ya mwekezaji na Msajili wa Hazina wa Hati zinazomwezesha mwekezaji kuendelea na kazi kumechelewesha uzalishaji katika kiwanda cha chuma. Wizara inafuatilia kwa karibu masuala hayo” aliongezea Mhe. Mbene

Mazungumzo kati ya Serikali na wamiliki wa viwanda vya Mbao na Chuma yalifanyika na kukubaliana jinsi ya wao kuanza upya kutekeleza wajibu wa kimkakati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...