Balozi Tuvako Manongi Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa akizungumza wakati wa uzinduzi wa onyesho la picha lililoandaliwa kwa ubia baina ya Wakilishi za Kudumu za Italia na Tanzania. Onyesho hilo linahusu huduma za afya ya mama na mtoto zinazotolewa na Taasisi isiyo ya kiserikali ya Doctors with Africa CUAMM katika hospitali ya Tosamaganga, Mkoani Iringa. Kushoto kwa Balozi Manongi ni Balozi wa Italia katika Umoja wa Mataifa, Bw. Sebastioano Cardi na kulina ni mmoja wa Wabunge kutoka Italia anayehudhuria mkutano wa 59 wa Kamisheni kuhusu Hadhi ya Wanawake.
Balozi Manongi akiteta jambo na Dkt. Andrea Atzori ambaye katika maelezo yake amesema taasisi hiyo ya Doctors with Africa CUAMM inampango wa kupanua huduma zake katika maeneo mengine ya pembezoni mwa Tanzania, mbali ya Tosamaganga na Mikumi.
Dkt. Andrea Atzori akiwa na Bi. Tully Mwaipopo, Afisa wa Uwakilishi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa mara baada ya uzinduzi wa onyesho hilo.
baadhi ya picha zinazoonesha huduma ya utoaji wa afya ya mama na mtoto katika Hospitali ya Tosamaganga , huduma hiyo ainayoendana manafumzo kwa wataalamu wa afya imeweza kuokoa maisha ya wanawake wajawazito pamoja na watoto wachanga wanaozaliwa kabla ya muda.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...