Mkuu wa Vodacom Tanzania,Kanda ya Tanganyika George Venanty(kushoto) na Meneja Masoko wa Kampuni ya Associate AEG Winnie Nyamubi(kulia) wakielezea matumizi ya Umeme Jua”Solar Power” wakati wakukabidhi msaada huo uliotolewa na Vodacom Foundation kwa wahanga wa maafa ya mvua kwenye kijiji cha mwakata wilayani Kahama Mkoani Shinyanga mwishoni mwa wiki.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga(kulia) akipokea msaada wa Umeme Jua ”Solar Power”kwa niaba ya wahanga wa maafa ya mvua uliotolewa na Vodacom Foundation kutoka kwa Mkuu wa Vodacom kanda ya Tanganyika,George Venanty.

Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania, kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii “Vodacom Foundation” leo imekabidhi msaada kwa wahanga wa mvua wa Kahama mkoani Shinyanga. Msaada huo unatokana na mchango wa kampuni na michango ya wateja wake walioguswa na tukio hilo kupitia  namba  maalumu ya kupokea msaada ya kusaidia majanga mbalimbali ya 155990.

Mvua kubwa iliyonyesha wilayani Kahama mkoani Shinyanga mapema mwezi uliopita ilisababisha vifo vya watu 42 na wengine mamia kujeruhiwa na kuacha familia nyingi zikiwa hazina makazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...