Mkurugenzi wa Ukaguzi wa ndani wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Godfrey Ngonyani (kushoto) akimkabidhi zawadi mtarishaji wa kipindi maarufu cha Power Breakfast Bw. Phillip Mwihava baada ya kumalizika kwa semina ambayo PSPF iliandaa maalum kwa watendaji kutoka Clouds Media. Lengo la semina hiyo ni kuwaelimisha kwanini PSPF inaendelea kuwa chaguo la kwanza kwa waajiriwa wapya hapa nchini. Anayeshuhudia Bibi. Neema Muro, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSPF.
Afisa uhusiano Mwandamizi wa Clouds Media Bw. Kelly Michael (kushoto) akisisitiza jambo wakati wa semina iliyoandaliwa maalum kwa watendaji wa Clouds Media, kulia ni Said Mohamed maarufu kama Bonge naye akifatilia kwa makini semina hiyo iliyolenga kuwaelimisha juu ya huduma na bidhaa mbalimbali za PSPF.
Watendaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF na wageni wao kutoka Clouds Media wakiwa katika picha ya pamoja baada ya semina iliyoandaliwa maalum kwa ajili ya watendaji wa Clouds Media.

Na Mwandishi Wetu

Mwanzoni mwa wiki hii wafanyakazi wa Clouds Media Group walipata fursa ya kutembelea Makao Makuu ya Mfuko wa Pensheni wa PSPF kwa lengo la kujengewa uwezo juu ya huduma mbalimbali zinazotolewa na PSPF. Ziara hiyo iligawanyika katika sehemu mbili, ya kwanza ilikuwa ni semina na ya pili ilikuwa kutembelea maeneo mbalimbali ya PSPF ili kuweze kujionea utendaji kazi wa Mfuko huo ambao kwa sasa ndio changuo la kwanza kwa waajiriwa wapya nchini.

Semina hiyo iliendeshwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSPF, Bibi. Neema Muro ambaye aliwaeleza kwa kina juu ya bidhaa na huduma zinazotolewa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF. Bibi. Muro alisema Mfuko wa PSPF una mafao ya muda mfupi ambayo ni fao la uzazi, mkopo wa elimu, fao la kujitoa, mkopo kwa mwajiriwa mpya, mkopo wa nyumba na mikopo kwa wastaafu yenye masharti nafuu. Aliyataja mafao ya muda mrefu kuwa ni fao la uzeeni, fao la ulemavu, fao la mirathi na fao la kufukuzwa au kuachishwa kazi.

Pia Mkurugenzi huyo alieleza kwamba PSPF ina mpango wa uchangiaji wa hiari ambao mwanachama wake ni mtu yeyote wenye umri wa miaka 18 na kuendelea na anaweza kuwa katika sekta rasmi na hata katika sekta isiyo rasmi, kima cha chini cha kuchangia nia shilingi 10,000 tu kwa mwezi. Mafao yanayotolewa chini ya mpango huu ni pamoja na Fao la elimu, Fao la ujasiriamali, fao la uzeeni, fao la kifo, fao la ugonjwa au ulemavu na fao la kujitoa.

Kwa upande wa uwekezaji, Bibi Muro alisema Mfuko una vitega uchumi vya muda mrefu ambavyo ni pamoja na jengo la Golden Jubille Towers lenye ghorofa 21 ambalo ndio Makao Makuu ya PSPF, Jengo la PSPF Commerial Towers ambalo lina ghorofa 35, jengo hili ni refu kuliko yote Afrika Mashariki na Kati. Pia PSPF imewekeza katika ujenzi wa Chuo cha Elimu cha Chuo Kikuu cha Dodoma na Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo Arusha.

Mfuko pia umejenga nyumba kwa ajili ya kukopesha wanachama wake na watanzania wengine katika mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam, Shinyanga, Mtwara,Tabora na Iringa. Baada ya semina hiyo wageni hao kutoka Clouds Media Group walipata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya PSPF kwa lengo la kujionea utendaji kazi wa Mfuko huo na pia kutembelea baadhi ya maeneo ya uwekezaji wa Mfuko.

Baada ya ziara hiyo, kiongozi wa timu kutoa Clouds Media, Bw. Kelly Michael alisema, “ ziara hii imetupatia elimu ya kutosha juu ya PSPF…hakika kuna mengi tulikuwa hatuyajui lakini sasa tunaweza kumepata uelewa wa kutosha juu ya Mfuko huu,”.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...