WAUMINI wa Kikristo waliopata fursa ya kushiriki semina ya neno la Mungu iliyoandaliwa na mtumishi wa Mungu Mwalimu Christopher Mwakasege iliyomalizika jana katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam wamesema wanahamu kubwa na Tamasha la mwaka huu kwa kuwa litakuwa na vitu vya kipekee.

Wakizungumza leo katika viwanja hivyo, walisema kikubwa ambacho kinaonesha utofauti ni kutimiza miaka 15 tangu kuanza hivyo kuadhimisha miaka hiyo kutakuwa na mambo tofauti yatakayopatikana siku hiyo.

Waumini hao walisema tamasha hilo ni kubwa hakuna tamasha lingine kubwa kama hilo ambako watanzania pia wanapata nafasi ya kuwaona waimbaji wakubwa wa ndani na nje ambao wamekuwa wakiwasikia tu sauti zao.

Walisema kuwa kuna njia tofauti za utoaji wa neno la Mungu ambako kwa njia ya uimbaji inawashawishi watu wengi hasa vijana kusikiliza nyimbo na hivyo inakuwa rahisi kumrudia Mungu  hali ambayo inachangia kupungua kwa vitendo viovu.


“Tunalisubiri kwa hamu kubwa Tamasha la mwaka huu maana linaonekana litakuwa kubwa na tofauti na yaliyopita kwa kweli waaandaji wawe na moyo huohuo wa kutuletea waimbaji mbalimbali wa kutoka nje tunafurahi kuwaona na pia tunapata upako mno tunapowaona wanahubili jukwaani” alisema  mmoja wa mashabiki hao Debora Kaduma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...