Mratibu wa Mradi wa MDOTS unoafanya utafiti wa tiba ya ugonjwa wa siko seli (Sickle Cell) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Robert Mongi (kulia) akifafanua jambo kwa baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania waliofika hospitalini hapo kukabidhi msaada wa simu 150 aina ya ZTE zitakazotumiwa na wagonjwa wa siko seli kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa za ugonjwa huo na kuzituma katika hospitali hiyo kila watumiapo dawa hizo kwa ajili ya kujua kama wanafuata matumizi sahihi ya dawa hizo.
Mkuu wa kitengo cha Vodacom Foundation Reenu Verma (kulia) akimfungulia boksi lenye moja ya simu kati ya 150 aina ya ZTE, Mratibu wa Mradi wa MDOTS unoafanya utafiti wa tiba ya ugonjwa wa siko seli (Sickle Cell) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt Robert Mongi wakati wa makadhiano ya msaada wa simu hizo zilizotolewa na mfuko huo kwa ajili ya wagonjwa wa siko seli kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa za ugonjwa huo na kuzituma katika hospitali hiyo kila watumiapo dawa hizo kwa ajili ya kujua kama wanafuata matumizi sahihi ya dawa hizo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania wakiwa wamebeba maboksi yenye simu aina ya ZTE walipofika kukabidhi msaada wa simu 150 zilizotolewa msaada na Vodacom Foundation katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya wagonjwa wa siko seli kujirekodi na kutuma video wakati wakimeza dawa za ugonjwa huo na kuzituma katika hospitali hiyo kila watumiapo dawa hizo kwa ajili ya kujua kama wanafuata matumizi sahihi ya dawa hizo.
BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI
Siko seli haina kiswahili chake, maana naona neno limetoholewa kutoka kiingereza. Chembe hai ya ...
ReplyDelete