Mchungaji wa mifugo akinywesha maji mifugo yake kwenye eneo lenye maji ambalo Waizri Prof. Maghembe amepiga marufuku kunywesha kwenye eneo hilo.

Na Hussein Makame-MAELEZO, Musoma

WAZIRI wa Maji Profesa Jumanne Maghembe amewaonya wananchi wanaoharibu vyanzo vya maji kwamba kufanya hivyo kunahatarisha uhai wa vyanzo hivyo.

Ametoa onyo hilo kwa nyakati tofauti wakati akiwa kwenye shughuli za kuweka mawe ya msingi kwenye miradi ya maji kwenye maeneo mbalimbali ya wilaya ya Serengeti mkoani Mara ambako Maadhimisho ya Wiki ya Maji kitaifa yanafanyika. 

 Akiwa katika kijiji cha Rung’abure, Waziri alishuhudia baadhi ya wafugaji wakinywesha mifugo yao kwenye maeneo ya vyanzo vya maji huku baadhi wakilima karibu na chanzo cha maji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...