Ujumbe mwingine uliokuwa kwenye mabango hayo.
Ujumbe mwingine ukinyesha kuwa toka Kijiji hicho kianzishwe mwaka 2008 na kupewa hati wananchi hao wamekuwa hawana haki na sehemu ya ardhi yao ambayo ipo ndani ya shamba la Muwekezaji huyo. 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Skaungu muda mfupi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Ardhi Mhe. William Lukuvi kuzungumzia lengo la ziara yake katika Kijiji hicho, alisema ni muda sasa kumaliza mgogoro huo.  

 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi (kulia) akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Skaungu leo tarehe 25/03/2015. Alisema kuwa mgogoro huo unawanyima usingizi viongozi wa Serikali na imefika wakati sasa kuumaliza. Aliongeza kuwa iwapo Serikali itaamua sehemu ya shamba hilo irudi kwa wananchi basi halitagawiwa kiholela na badala yake utatumika utaratibu maalum kwa kushirikisha Halmashauri na Serikali ya Kijiji kwa kuanza kuwatambua wale wenye hitajio kubwa la ardhi na baadae kuwaangalia wananchi wengine wenye haki ya kupatiwa maeneo hayo.
 Wadau wa Habari Mkoa wa Rukwa wakitoka kuchukua matukio katika Kijiji cha Skaungu, Kutoka kulia ni Juddy Ngonyani (Channel Ten), Nswima Errrrrnest (TBC), Joshua Joel (ITV), Peti Siame (Habari Leo/Daily News), Gurian Adolph Ndingala FM na Mussa Mwangoka (Mwananchi).
 Bi. Anna Msafiri Mwananchi wa Kijiji cha Mawenzusi akitoa kero yake kwa Mhe. Waziri wa Ardhi.
Sehemu ya wananchi wa kijiji cha Mawenzusi ambao pia walipata fursa ya kupaza sauti zao kwa Waziri wa Ardhi Mhe. William Lukuvi. Picha  zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...