![]() |
Jerry MuroMsemaji wa Timu ya Yanga |
Na Ripota wa Globu ya Jamii
Uongozi wa Klabu ya Yanga umeishukia bodi ya Ligi kwa kile walichodai kuwa wamechakachua kanuni kwa kuiruhusu Timu ya Simba kumtumia mchezaji Ibrahimu Hajibu na kuitaka sheria zichukue mkondo wake huku wakigomea mechi yao dhidi ya JKT Ruvu kusogezwa mbele.
Akizungumza kwenye Makao Makuu ya Klabu hiyo leo, Msemaji wa Yanga Jerry Muro amesema Bodi ya Ligi inayumbisha soka la Tanzania kwa kupindisha sheria na kitendo walichofanya ni cha ubabaishaji na hawawezi kukikalia kimya.
"Umeshaona wapi mtu anakosa, anakaa kujadili adhabu ya kupewa na mtoa adhabu, Tanzania ni ya kwanza, halafu eti tunataka soka letu lisonge mbele, litasonga mbele kwa stahili hii?"alisema kwa kuhoji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...