Wakazi wa  eneo la Kwa Mangi kata ya Kibosho Kati  wakimsikiliza   Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipokuwa akiwahutubia,Kinana aliwaeleza wananchi hao kuwa kuna baadhi ya watu wanaotaka nafasi za Uongozi wamekuwa wakijipitisha pitisha kuomba uongozi,hivyo amewaonya na kuwatahadharisha kutojipitisha pitisha kugombea nafasi za uongozi kabla ya muda kuisha na kutangazwa.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa  Kwa Mangi kata ya Kibosho Kati ambapo aliwaambia wananchi waache kujipitisha pitisha kugombea nafasi za uongozi kabla ya muda kuisha na kutangazwa.
 Baadhi ya Kadi zaidi ya 335  za wanachama walizozikabidhi kwa Ndugu Kinana na wamejiunga na CCM kwenye mkutano wa hadhara.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki uvunaji wa mpunga kwenye skimu ya umwagiliaji ya Lower Moshi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupanda mti wa kumbukumbu kwenye chuo cha Ufundi KVTC,Kibosho wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro.
  Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini Ndugu Cyril Chami akihutubia wananchi wa kijiji cha Chekereni kata ya Mabogeni. Kata ya Mabogeni ina vijiji 8 na vyote vimeshinda kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa. Jimbo la Moshi Vijijini lina Kata 16 ,shule za sekondari zilizojengwa ni 29.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kijiji cha Chekereni kata ya Mabogini.

PICHA NA MICHUZI JR-MOSHI VIJIJINI 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mimi kawaida huwa namfagilia sana Mh Kinana ila leo inabidi niulize, hizo kadi mbona kama zote ni mpya??

    Che

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...