Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kijiji cha Misisi kata ya Misisi,wilayani Bahi mapema leo,mkoani Dodoma akiwa ziarani ndani ya jimbo la Bahi.

Ndugu Kinana amezungumza na wananchi hao waliokuwa wamebeba mabango na kuzuia msafara wake,kutokana na matatizo yaliyokuwapo katika kijiji hicho na kukosa ufumbuzi kwa muda mrefu.Wananchi hao walikuwa na lalamiko lao moja kubwa lililohusu shule yao ya msingi ya Msisi,ambayo madarasa yake mawili yaliezuliwa paa (kama yaonekanavyo pichani) na mengine kubomoka kabisa kufuatia mvua kubwa ilionyesha na kusababisha madhara hayo.

Shule hiyo ya msingi Msisi ilipatwa na dhahma hiyo mnamo mwaka 2011,na mpaka leo haikuwahi kufanyiwa ukarabati wa aina yoyote huku walimu na wanafunzi wakipigwa na jua wakati wa masomo.Ndugu Kinana baada ya kusikiliza lalamiko hilo kutoka kwa wanakijiji hao,alianzisha harambee ya papo kwa papo iliyohusu viongozi wa CCM mkoa na Wilaya waliokuwa kwenye msafara huo na kuichangia shule hiyo na kufanikiwa kupata fedha na vifaa vya ujenzi ambavyo vitapelekea kuanza upya kwa ujenzi wa madarasa  hayo,Aidha Wananchi wa kijiji hicho walimshukuru Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana kwa harambee alioifanya na kupelekea kupatikana kwa misaada hiyo.

Ndugu Kinana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wapo kwenye ziara ya siku tisa mkoani Dodoma ya kukagua,kuhimiza na kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2010 pamoja na kusikiliza matatizo ya wananchi na kuyatafutia ufumbuzi.Kinana leo amemaliza ziara yake ndani ya jimbo la Bahi kesho kuunguruma kondoa.
 Mmoja wa wananchi wa kijiji cha Msisi akiwa amebeba bango lake kichwani.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akisoma moja ya bango lililokuwa limebebwa na mmoja wa wananchi wa kijiji cha Msisi,Wilaya ya Bahi lililohusu shule ya msingi ya kijiji hicho kukosa madarasa ya kusomea wanafunzi,kufuatia mvua mkubwa kuezua mapaa.
  Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana,Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Mh Chiku Galawa na Mbunge wa Jimbo la Bahi,Mh Omari Badwel wakishiriki uchimbaji wa mitaro na kufukia bomba za maji,katika kijiji cha Nguji kata ya Mundemu wilaya ya Bahi mkoani Dodoma.Mradi huo wa maji unatarajiwa kuhudumia zaidi ya watu elfu tatu,aidha mradi huo uliogharimu kiasi cha fedha zaidi ya Milioni mia saba unatarajiwa kukamilika Aprili 15,2015.
 Wanachi wa kijii cha Chonde wakishangilia wakati Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipokabidhiwa Mkuki na kuvalishwa mgolole ikiwa ni ishara ya kuwa mmoja wa wazee wa kijiji hicho cha Chonde.
  Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Chonde wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipowahutubia jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara,wilayani Bahi mkoa wa Dodoma.

PICHA NA MICHUZI JR-BAHI

HABARI PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. MH. ABDULLAHAMAN KINANA, NDIYE ANAYE STAHILI KUWA RAIS WA TANZANIA AWAMU INYOFUATA, NI MCHAPAKAZI WA KUTISHA NA NDO ANAYE IFANYA C.C.M IWE HAI.VERY GOOD I LOVE HIM.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...