Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana (wa pili kulia)akishiriki ujenzi wa tanki la
maji katika Kijiji cha Sakala, wilayani Ngorongoro.Ndugu Kinana na
ujumbe wake wako kati wa ziara ya
siku tisa mkoani Arusha ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua miradi inayotekelezwa kwa kufuata
Ilani ya Uchaguzi ya CCM, pamoja na kusikiliza kero za Wananchi na
kuzitafutia ufumbuzi.
Komredi
Kinana akisaidiana na Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro, Telele kujenga
vyumba vya madarasa ya kidato cha nne na cha tano katika Shule ya
Sekondari Samunge, wilayani Ngorongoro.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM
kijiji cha Wasso Ndugu Revocatus William Parapara. Awali ndugu
Revocatus William Parapara alikuwa Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya
Ngorongoro kwa takribani miaka 15.
Akijibu hoja zao Ndugu Abdulrahman Kinana amesema hawezi kujibu lolote kwa sasa ili asije kuonekana amedanganya. lakini ameahidi kurudi kijijini hapo baada ya mwezi mmoja mara baada ya kukutana na Mawaziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii na Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi na kupata taarifa juu ya ahadi ya Waziri Mkuu pamoja na viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro, Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro pamoja na mhifadhi wa Ngorongoro ili kuzungumzia suala hilo kwa ajili ya kupata ufunbuzi wa kudumu.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akikabidhi mbuzi kutoka kwa
baraza la Wafugaji kwa Wananchi wasiojiweza ili kupambana na baa la njaa
linalowanyemelea.Kila kaya ilikabidhiwa mbuzi 15,ambapo idadi ya mbuzi
wapatao 2470 walikabidhiwa kwa wananchi hao na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu
Kinana.
Komredi Kinana akigawa
mbuzi bure kwa wajane kila kaya mbuzi 15 zilizotolewa na Baraza la
Wafugaji Ngorongoro kwa kushirikiana na Hifadhi ya Ngorongoro ili
kuwapunguzia watu hao umasikini.
Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin
Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin
akigawa mbuzi bure kwa
wajane kila kaya mbuzi 15 zilizotolewa na Baraza la Wafugaji Ngorongoro
kwa kushirikiana na Hifadhi ya Ngorongoro ili kuwapunguzia watu hao
umasikini.
Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin
Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin
Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwahutubia wanakijiji cha
Naoinokanoka,Wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha mapema leo,Kinana pamoja
na kuwahutubia wananchi hao pia aliruhusua kuulizwa maswali mbalimbali
likiwemo suala la mipakya ya hifadhi ya Ngorongoro na vijiji vyao,ambapo
pia hawaruhusiwi hata kulima zao la aina yoypte kwenye makazi yao
Aidha walieleza kuwa Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda aliwahi kufanya ziara katika kijiji
hicho na kuahidi kuwa serikali itatoa magunia 10 ya mahindi kwa kila kaya
kwa mwaka ili kupunguza makali ya njaa kutokana na ukame, Jambo ambalo
halijatekelezwa mpaka sasa.
Akijibu hoja zao Ndugu Abdulrahman Kinana amesema hawezi kujibu lolote kwa sasa ili asije kuonekana amedanganya. lakini ameahidi kurudi kijijini hapo baada ya mwezi mmoja mara baada ya kukutana na Mawaziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii na Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi na kupata taarifa juu ya ahadi ya Waziri Mkuu pamoja na viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro, Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro pamoja na mhifadhi wa Ngorongoro ili kuzungumzia suala hilo kwa ajili ya kupata ufunbuzi wa kudumu.
PIchani
ni baadhi ya Viongzi wa Baraza la Wafugaji,Viongozi wa Mamlaka ya
hifadhi ya Ngorongoro na wazee wa Kimila wakimsikiliza katibu Mkuu wa
CCM,Ndugu Kinana kuhusiana na mambo mbalimbali yahusuyo ardhi
Picha
Kati ni Ndugu Kinana akiwa na baadhi ya viongozi wa chama wakishiriki
kupaka rangi jengo la nyumba ya mganga katika kijiji cha Bulati,wilayani
Ngorongoro.
PICHA NA MICHUZI JR-NGORONGORO.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...