MADAKTARI bingwa kutoka hospitali ya  SPS Apollo iliyopo  Ludhiana
nchini India wamewasili nchini na kuanza kutoa huduma ya ushauri bure
kwa magonjwa makubwa ambayo yamekuwa yakiwasumbua watu wengi na
kuwalazimu  kwenda kutibiwa nchini India.

Akizungumza na waandishi wa habari katika kituo cha kutoa huduma kwa
matibabu Arusha, Austin Makani alisema kuwa , madaktari bingwa hao
wanatoa ushauri kwa wagonjwa wenye matatizo ya Figo , Moyo, tumbo,
saratani, mishipa ya fahamu, uti wa mgongo, upasuaji wa kawaida na wa
kupunguza uzito.wanawake (MMC) ambapo ushauri huo unatolewa, Mratibu wa Kambi hiyo ya

Austin alisema kuwa,  ujio wa madaktari hao watano kutoka  nchini
India umeratibiwa na kituo  cha kutoa huduma kwa wanawake (MMC) kwa
kushirikiana na hospitali ya SPS Apollo iliyopo Ludhiana nchini India
na wamefikia hatua hiyo baada ya kugundua kuwa wagonjwa wengi
wanaoenda kutibiwa nchini India wanasumbuliwa na magonjwa hayo.

Alisema kuwa, uwepo wa madaktari hao bingwa kwa siku tatu utasaidia
sana wananchi wa jiji la Arusha kufika na kupewa ushauri bure juu ya
magonjwa yanayowasumbua na hivyo kuokoa gharama ya kusafiri hadi
nchini India kufuata huduma hizo.

‘hapa sisi wanachofanya madaktari hawa bingwa ni kusikiliza wagonjwa
na baada ya kupata maelezo wanapata ushauri bure wa kwenda kupima
kulingana na ugonjwa alionao na baada ya kurudisha majibu ndipo
tunamwandikia dawa ya kutumia na kama ugonjwa wake unahitaji kutibiwa
India tunampunguzia  gharama  kidogo ya kwenda kutibiwa India ‘alisema
Austin.

Alisema kuwa, uwepo wa kambi hiyo ya matibabu jijini Arusha unatoa
fursa pia kwa wagonjwa waliokuwa wakatibiwe nchini India kutokana na
magonjwa yanayowasumbua na kuweza kupata ushauri wa haraka na wakti
mwingine kuepuka gharama za kusafiri.

Wakizungumza  katika kituo hicho, Madaktari hao bingwa ,Abhijit Singh
na Atul Behll kutoka hospitali ya SPS Apollo India  walisema kuwa
,changamoto kubwa iliyopo katika nchi za kiafrika ni watu wengi
kutokuwa na utamaduni wa kwenda kupima afya zao ,hivyo aliwataka
wananchi wa mkoa wa Arusha na mikoa jirani kufika kwa wiki ili kupata
ushauri juu ya afya zao.

Walisema kuwa,nchini India  kuna watanzania wengi wanaopata matibabu
kwa wao kuwafikia na kuweza kutoa ushauri bure na hatimaye kupunguza
gharama za kwenda nchini India.kutokana na magonjwa yaliyotajwa ,hivyo wakaona kuna umuhimu mkubwa.
SAM_2088
Wagonjwa wakiwa wanapatiwa vipimo mbalimbali .
SAM_2082
Atul Behll ambaye pia ni daktari bingwa kutoka India akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari.
SAM_2097
Mgonjwa aliyekuja kupata huduma akiwa anasaidiwa na wahudumu wa kituo hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...