Na Bashir Yakub.
Suala la matunzo haliishi tu kwa mtoto/ watoto. Wengi wa wanaume wamekuwa wakipendelea kuwajibika kwa kutoa matunzo ya watoto na kumuacha mwanamke. Jambo hili si sawa na halikubaliki kisheria. Ni vema kufahamu kuwa suala la matunzo kwa mwanamke limegawanyika mara nne. Kwanza kuna matunzo kipindi ambacho ni cha ndoa ambapo hakuna mgogoro wowote baina ya wanandoa. Pili kuna matunzo kwa mwanamke kipindi ambacho wanandoa wanakuwa wametengana lakini hawajatalikiana. Tatu kuna matunzo kwa mwanamke kipindi ambacho kuna mgogoro wa familia mahakamani, na nne matunzo kwa mwanamke kipindi ambacho talaka imekwishatolewa.
1.MATUNZO YA MWANAMKE WAKATI WA NDOA.
Hiki ni kipindi ambacho ndoa huwa inaendelea vyema bila kuwapo kwa mgogoro wa aina yoyote ambao unaweza kutishia uwepo wa ndoa hiyo. Katika kipindi hiki mwanaume ana wajibu wa kisheria kutoa matunzo kwa mke wake. Hii ni kwa ndoa zote yaani zile za kimila, kiserikali, kidini ikiwemo ile ya kuishi wote kwa zaidi ya miaka miwili ( presumed marriage). Mwanaume yeyote ambaye anaishi na mwanamke katika ndoa mojawapo kati ya hizi basi huyo anawajibika kutoa matunzo kwa mwenza wake.
2.MATUNZO KWA MWANAMKE KIPINDI AMBACHO AMETENGANA NA MME WAKE.
Kisheria kuna tofauti kubwa kati ya kutengana na kutalikiana. Kutengana ni kutengana na inaweza kuwa waliotengana wanaishi nyumba moja lakini vyumba tofauti au vitanda tofauti. Lakini pia inawezekana waliotengana wakawa wanaishi nyumba tofauti na sehemu mbali kabisa. Huku kote ni kutengana wala sio kutalakiana au kuachana. Kwa hiyo wanaume walio katika kipindi cha kutengana na wake zao wanawajibika kutoa matunzo kwa wanawake hao. Hii ni kwa mujibu wa sheria wala si vinginevyo. Haki ya mwanamke kutunzwa inabaki palepale japo hukai nae chumba kimoja, hauli chakula chake, haukai nae nyumba moja, na wala hamshirikiana chochote. Hii ina maana kuwa kutoshirikiana naye katika haki yoyote ya ndoa hakuondoi wajibu wa kisheria wa kutoa matunzo kwa mwanamke huyo. Katika kipindi hiki cha kutengana ni makosa kukataa kumtolea matunzo mwanamke.
Hii sheria imepitwa na wakati, kwanini mwanamke atunzwe kwani hawezi kujitunza ? , you can`t have both ways, wanataka na wamepewa equal opportunities, halafu tena tuwatunze kwani wao watoto, wazee au hawajiwezi?
ReplyDelete