Na  Bashir  Yakub.
Kumekuwa  na  tabia  ya  taasisi  za  fedha  kuuza  nyumba   au  viwanja vya  watu  walivyoweka  rehani   na kushindwa  kulipa  mkopo   kwa  bei  ya  kutupa. Kwakuwa  taasisi  za  fedha  huamini  kwamba  wana  deni na  mtu  na ameshindwa  kulipa  hela  zao  na  pengine  kwakuwa  tayari  wamekamilisha  taratibu  zote  za  kisheria  za  kuuza  basi  huamua  kuuza  mali  ya  mtu  kwa  bei   ambayo    ni  ndogo   kiasi  cha  kustaajabisha.  

 Ni  kawaida  kukuta  nyumba ya  milioni  mia  ikiuzwa  hata  milioni kumi  na  tano  ili  kulipia  deni  la  milioni  kumi  na mbili  au  kumi  na  tano.  Watu  wanapaswa kuelewa  kuwa hili  si  sawa  na  sheria  imekataza    jambo  hili. Thamani  ya  nyumba  au  kiwanja  iko  palepale  hata  kama  mtu  ameshindwa  kulipa  mkopo.  Si  kweli  kuwa  kwakuwa  sheria  imeruhusu  kuuza  mali  ya  mtu  anaposhindwa  kulipa  mkopo   basi  imeruhusu   kuuza  bei  yoyote  ile  ilimradi  muuzaji  amepata   kiasi  anachodai.  Hili  si  kweli  kama  tutakavyoona  hapa  chini. 

1.WAJIBU  WA  TAASISI  YA  FEDHA  KATIKA  KUUZA  NYUMBA  YA  DHAMANA.  . 
Kwa  kujua  hili  la  kuuza  mali  za  watu  bei  ya  kutupa  Sheria  ya  ardhi  kifungu  cha  133  ( 1 ) kikasema  kuwa  muuzaji  wa  nyumba  iliyowekwa  rehani   ana  wajibu  mkubwa  na  wa  hali  ya  juu  kuhakikisha  anachukua  tahadhari  na  anakuwa  mwangalifu  kwa  kiwango  cha  juu  kuhakikisha    wakati  anapouza   ardhi   ya  mtu anaiuza  kwa  bei  nzuri   na  bei  ambayo  inakubalika  kuwa  bei  inayostahili  kwa  wakati husika.  

Huu  ni  wajibu  wa  kisheria  alionao  muuzaji  au  mnadishaji  wa  ardhi  ya  dhamana.  Kifungu  hicho  kinasema  kuwa  suala  la  kuuza  mali  ya  dhamana  kwa  bei  inayokubalika  ni  haki  ambayo  aliyeshindwa  kulipa  deni  anamdai  muuzaji/mnadishaji.  Kwa  hiyo  wewe   unayedaiwa  unamdai  huyo  mnadishaji  anayetaka  kuuza  nyumba  yako  haki  ya  kuuza  hiyo nyumba   katika  bei  inayokubalika ( reasonable  price). 

2. NYUMBA/KIWANJA  KIUZWE  BEI  GANI  KWA  MUJIBU  WA  SHERIA ? 
Sheria   ya  ardhi  haikutaja  moja  kwa  moja   ni  kiasi  gani nyumba   ya  mtu  au  kiwanja  kinatakiwa kuuzwa. Hii  ni  kutokana  na  utofauti  wa  thamani  wa  mali  hizo  na  hivyo  isingekuwa  rahisi  kusema  kuwa  bei  ya  mwisho  ya  nyumba  au  kiwanja  ni  kiasi  fulani.  Ili  kuliweka  sawa  hili  kifungu  hichohicho  cha  133( 2 ) kikasema  kuwa   nyumba/kiwanja  cha  mtu   hakitakiwi  kuuzwa    25%    ya   bei  ya  soko   ya  nyumba  au  kiwanja   hicho  kwa  wakati  huo  au  chini  yake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...