Mkuu wa Mkoa wa Kagera wa sasa Mheshimiwa John V.K. Mongella ukimuaga aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Kagera wa 20  Kanali Mstaafu Fabian Inyasi Massawe kwa jina maarufu Mulokozi.
Tangu uhuru  wa iliyokuwa Tanganyika sasa Tanzania  mwaka 1961 miaka 53 ya uhuru mkoa wa Kagera umekuwa ukiongozwa na viongozi mbalimbali hasa katika nafasi ya  ukuu wa mkoa na kwa kipindi hicho chote hadi sasa tayari mkoa umeongozwa na wakuu wa mikoa wapatao 21 kwa vipndi  tofauti.
Viongozi hao  (Wakuu wa Mkoa)  waliowahi kuuongoza mkoa wa Kagera kwa nyakati  tofauti  waliweza kuisogeza Kagera kutoka katika hali fulani na kupiga hatua kimaendeleo katika nyanja  mbalimbali ikiwa ni pamoja na uchumi, elimu,  siasa, utamaduni, miundombinu, na nyanja mbalimbali za ustawi wa jamii.
Mkoa wa Kagera chini ya uongozi wa Mkuu wa Mkoa wa sasa Mheshimiwa John V.K. Mongella ulimuaga aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Kagera wa 20 na aliuongoza  mkoa  kwa miaka mitatu akiteuliwa kutoka katikanafasi ya Ukuu wa Wilaya ya Karagwe naye ni Kanali Mstaafu Fabian Inyasi Massawe kwa jina maarufu Mulokozi.
Kama walivyokuwa watangulizi wake Mhe. Kanali Mstaafu Massawe alifanya mengi katika mkoa wa Kagera na kuweka rekodi ya mambo mengi aliyoyafanya yakiongozwa na kaulimbiu yake ya “Amani na Maendeleo” kubakia katika kumbukumbu za mkoa wa Kagera na wananchi wake kwa ujumla.
Kupata historia ya Kanali Mstaafu Fabian Inyasi Massawe BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...