Waziri wa Mambo ya Nje wa Zamani wa Marekani  Mama Hillary Clinton akiwa na wenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwa Ikulu Dar es salam wakati alipotembelea Tanzania June 13, 2011.
Imetangazwa leo kuwa Mama Clintoameamua kujitosa katika kuwania nafasi ya Urais wa nchi hiyo mwakani. John Podesta, Meneja wa kampeni wa Clinton leo katuma email kwa wanaomuunga mkono, kwamba  Clinton yumo katika mbio hizo,
Podesta amesema  Clinton anaelekea Iowa kukutana na wapiga kura na kwamba sherehe rasmi ya kutoa tamko itafanyika mwezi ujao.
Akiongea kwenye video fupi iliyo kwenye tovuti yake rasmi ya kampeni, amesema" Mimi natagombea urais, Wamarekani wamepigana na kigingi cha hali ngumu ya uchumi lakini karata  bado iko mikononi mwa walio juu. Kila siku Wamarekani wanahitaji bingwa, nami nataka kuwa huyo bingwa ili tuweze kufanya zaidi ya kupita tu. Inawezekana kuwa mbele na kubakia mbele, Sababu pale familia zinapokuwa na nguvu, Marekani ina nguvu.
"Hivyo naingia barabarani kupata kura zenu, Sababu huu ni muda wenu na namini mtaungana nami katika safari hii" amesema kwenye video hiyo ambayo ukitaka kuiona kwenye tovuti yake.... 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hata wakina mama nao wanaweza mwache apambane, ana ujuzi na uzoefu wa kutosha akipata anaweza kuwa kiongozi mzuri tu wa nchi kubwa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...