Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(kulia)akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati
wa kuchezesha droo ya 55 ya promosheni ya Jaymillions inayoendeshwa na kampuni hiyo iliyofanyika leo,ambapo
Habibu
Saidi(19)ambaye ni mkazi wa Kabale Bukoba vijijini anayesubiria kuanza
kidato cha tano hivi karibuni kwa kujishindia kitita cha shilingi
milioni 10.Kutoka
kushoto ni Msimamizi wa bodi ya michezo ya kubahatisha,Mrisho Millao na
Meneja wa huduma za ziada wa kampuni hiyo Mathew Kampambe.Ili mteja
kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno
Jay kwenda 15544 au AUTO kwenda namba hiyo iwapo simu haina fedha ambapo mteja
akiweka fedha anakatwa shilingi 300/-tu.
Zaidi ya milioni 300/-zimesha nyakuliwa na wateja walioshinda
Watanzania
wapatao 44 maisha yao yameweza kubadilika kutoka hali ya kawaida na
kuwa mamilionea kutokana na kujishindia fedha taslimu
kupitia promosheni ya siku 100 ya Jaymillions inayoendeshwa na Vodacom
Tanzania ambayo ilianza katikati ya mwezi Februari na inatarajia kufikia
ukingoni mapema mwezi ujao.
Hadi
kufikia sasa wateja wa Vodacom walioshinda wamejinyakulia shilingi
milioni 278 huku mamilioni mengine ya fedha yakisubiri kunyakuliwa
na washindi watakaobahatika katika siku chache zilizobaki kabla ya
promosheni kufikia tamati.
Meneja
Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu amesema promosheni bado
inaendelea na kuwataka watanzania waendelee kuangalia namba zao kama
zimeshinda kwa kutuma neno JAY kwenda namba
15544. Aliitaja njia nyingine ya kushinda kuwa ni kutuma neno
AUTO kwenda namba 15544 iwapo simu haina fedha ambapo mteja akiweka
fedha anakatwa shilingi 300/-
“Promosheni
ya Jaymillions inaendelea hivyo tunawakumbusha wateja wetu kuwa bado
kuna mamilioni ya kujishindia hivyo wachangamkie
kwa kujaribu bahati zao katika siku hizi ambazo promosheni inaelekea
ukingoni.Tunajivunia kwa kufanikiwa kubadilisha maisha ya baadhi ya
wateja wetu walioshinda wengi wakiwa ni wateja wenye maisha ya kawaida
na hii ndio dhamira yetu kubwa inayoendana na kauli
mbiu yetu ya “ukiwa na Vodacom maisha ni murua”. Nkurlu alisema
hayo wakati wa kuchezesha droo ya 55 iliyomwibua Habibu Saidi(19)ambaye
ni mkazi wa Kabale Bukoba vijijini anayesubiria kuanza kidato cha tano
hivi karibuni kwa kujishindia kitita cha shilingi
milioni 10.
Baadhi
ya wateja waliobahatika kushinda wanasema kuwa promosheni hii
imewafanya kutimiza ndoto zao zilizoshindwa kutimia kwa muda mrefu
kwa kuwa maisha yao yamebadilika kutoka hali duni kuwa bora zaidi.
Upendo
Madengenya kutoka wilayani Kilolo ambaye alikuwa mhudumu katika nyumba
ya kulala wageni wilayani humo ambaye alijishindia milioni
100 anasema“Jaymillions naifananisha na methali ya Kiswahili ya
kulala maskini ukaamka tajiri kwa kuwa nilikuwa nakabiliwa na changamoto
nyingi za maisha pamoja na familia yangu ,Mungu kaniona nikafanikiwa
kushinda hivi sasa maisha yangu yamebadilikakutoka
hali duni kuwa bora na bado safari ya kuelekea kwenye maisha bora zaidi
inaendelea.
James
Mangu kutoka Mwanza ambaye alijishindia milioni 10 anasema kuwa kwa
muda mrefu alikuwa anawaza kupata mtaji wa kuendeleza biashara
zake ndogo ndogo na kwa bahati nzuri ameweza kuibuka na ushindi na
kupata mtaji ambao anakiri kuwa utabadilisha maisha yake na familia yake
kwa ujumla kutoka maisha duni kuwa bora.
Hynes Petro Kanumba mkazi wa Rukwa anasema:”Katika
maisha yangu sitaisahau Vodacom Kwa kuwa kupitia promosheni yake ya
Jaymillions
imeniwezesha kunitoa katika hali duni na kuwa na maisha bora pamoja na
familia yangu na natoa wito kwa watanzania kutozipuuza promosheni hizi
kwa kuwa ni za kweli na zinalenga kutukomboa sisi wanyonge”
Kwa upande wake Deborah Stanley mshindi wa milioni 10 anasema:
“Nimefuatilia Promosheni ya Jaymillions naona inalenga kuwakomboa
kimaisha
watanzania hususani wenye kipato cha chini hasa wajasiriamali wadogo
wadogo kama vile; wamachinga, mama ntilie, wanafunzi na wazee wastaafu
ambapo kwa kiasi kikubwa tunajua watu wa aina hii wanahitaji msaada ili
kujiendeleza kiuchumi. Kwa fedha ambazo baadhi
ya washindi tayari wamezipata wengi zimewasaidia kujikwamua na
kujiendeleza kimaisha,".
Hongera Habibu kwa ushindi huu, acha maela yaendelee kutolea watu wapate mitaji ili mamilionea waongezeke.
ReplyDelete