01
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Mstaafu wa Marekani Mhe Bill Clinton Ikulu jijini Dar es salaam leo April 28, 2015.na kisha kufanya mazungumzo na rais huyo wa 42 wa Marekani yuko nchini  kukagua miradi ya maendeleo na afya inayofadhiriwa na taasisi za Clinto Development Initiative (CDI) na Clinto Health Access Initiative (CHAI).
2
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe Bill Clinton Ikulu jijini Dar es salaam leo April 28, 2015.rais huyo wa 42 wa Marekani yuko nchini  kukagua miradi ya maendeleo na afya inayofadhiriwa na taasisi za Clinto Development Initiative (CDI) na Clinto Health Access Initiative (CHAI).PICHA NA IKULU
---------------------------
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumanne, Aprili 28, 2015, amekutana na kufanya mazungumzo ya faragha na Rais wa 42 wa Marekani, Mheshimiwa Bill Clinton ambaye anafanya ziara nchini. 
Baada ya mazungumzo hayo, viongozi hao walipata chakula cha mchana cha pamoja kabla ya kiongozi huyo wa Marekani kuondoka Ikulu, Dar es Salaam.
 Katika mazungumzo hayo, viongozi hao wawili walizungumzia baadhi ya miradi ambayo inadhaminiwa na kugharimiwa na Taasisi ya Clinton Foundation katika nyanja ya afya na hasa katika maeneo ya utoaji wa dawa za kurefusha maisha kwa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi, afya za akina mama na jinsi ya kupunguza vifo vya watoto wadogo chini ya miaka mitano na jitihada za kupambana na malaria, Nyanja ya kilimo hasa uzalishaji wa mbegu kwa wingi na kilimo cha soya.

Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.

28 Aprili,2014


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...