Wanajeshi wa nchini Nepal wakiwa wamebeba misaada kwaajili ya wahanga wa tetemeko la ardhi

Kwa Msaada  wa mtandao.
Serikali ya Nepal imejitetea dhidi ya malalamiko juu ya misaada ya dharura, kufuatia tetemeko kubwa la ardhi  lililotokea Jumamosi  nchini humo.

Mkuu wa masuala ya dharura wa Nepal,Rameshwor Dangal,ameambia BBC serikali inajitahidi iwezavyo, lakini mkasa huo ulikumba majimbo 20 nchini humo na hivyo mahitaji ni mengi sana ndiposasa serikali inaelemewa.

Hali ya kutamauka imewakumba wengi waliothiriwa na tetemeko hilo,na wengine wameonesha malalamiko yao kwa kulumbana na polisi huko Kathmandu, mji mkuu wa taifa hilo.

Angalau sasa misaada ya bidhaa muhimu na huduma zimeanza kuwafikia waavijiji katika mji wa Kathmandu nchini humo.

Wakati huo huo, Mwanamme aliyetolewa ndani ya kifusi katika hoteli iliyoporomoka mjini Kathmandu ameelezea jinsi alivyoweza kuishi kwa saa 82 kabla ya kuokolewa.

Rishi Khanal amesema alilazimika kunywa mkojoo wake wakati akisubiri kuokolewa.

Mguu wake alikwama ndani ya kifusi lakini aliweza kuwasiliana na jamaa zake akitumia simu yake ya mkononi.

Hata hivyo hakumbuki hoteli alimokuwa, aliokolewa na makundi ya uokoaji kutoka nchini humo na Ufaransa.

Zaidi ya watu 5000 wamepoteza maisha katika janga hilo la tetemeko la ardhi huko Nepal.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...