Meneja wa Bia ya Safari Lager, Edith Bebwa(kushoto) na Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Polisi, Gerald Ngiichi wakimkabidhi kikombe mchoma nyama mkuu wa Bar Soccer City ya Sinza, Said Dando mara baada ya kuibuka mabingwa katika mashindano ya Safari Lager Nyama Choma jijini Dar es Salaam yaliyofanyika katika viwanja vya Leaders mwishoni mwa wiki.
Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Polisi, Gerald Ngiichi(wa pili kushoto) wakimkabidhi kitita cha Shilingi 1,000 ,000/= mchoma nyama mkuu wa Bar Soccer City ya Sinza, Said Dando mara baada ya kuibuka mabingwa katika mashindano ya Safari Lager Nyama Choma jijini Dar es Salaam yaliyofanyika katika viwanja vya Leaders mwishoni mwa wiki.Kushoto ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Edith Bebwa.

Na Mwandishi Wetu.

SOCCER City Bar yenye makazi yake Sinza jijini Dar es Salaam wameibuka mabingwa katika fainali za mashindano ya Safari Lager Nyama Choma 2015 yaliyofanyiaka mwishoni mwa wiki katika Viwanja vya Leaders Klabu na hivyo kuzawadiwa fedha taslimu Shilingi milioni moja na Kikombe.

Nafasi ya pili ilichukuliwa Chamanzi Bar ya Mbagala ambayo ilizawadiwa pesa taslimu Shilingi 800,000/=,nafasi ya tatu ni Liquid Barya Chang’ombe ambayo ilizawadiwa pesa taslimu Shilingi 600,000/=,nafasi ya nne ni High Way Bar ya Boko ambayo ilizawadiwa Shilingi 400,000/=, nafasi ya tano ni Amaholo Bar ya Salasala ambayo ilizawadiwa Shingi 200,000/- na nafasi ya sita ni Kilwa road Bar ambayo ilizawadiwa pesa taslimu Shilingi 100,000/=.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...