Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu baadhi ya Shule za Sekondari za Bweni  zilizofungwa kutokana na ukosefu wa chakula ambapo alisema shule hizo zimefungwa kimakosa kwani Serikali imeshapeleka fedha za kununulia chakula kwenye halmashauri zote nchini. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Elimu TAMISEMI Bw. Zuberi Samataba.
 Naibu Katibu Mkuu Elimu TAMISEMI Bw. Zuberi Samataba akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam mpango wa Serikali kuajiri waalimu wa shule za msingi wenye elimu ngazi ya Stashahada badala ya Cheti kama ilivyo sasa. Kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu ajira kwa walimu wapya waliohitimu 2014/2015 na kutoa rai kwa waalimu hao kwenda kuripoti kwenye vituo vya kazi watakavyopangiwa.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini wakati wa mkutano uliofanyika leo kwenye ofisi za TAMISEMI  jijini Dar es Salaam. Picha na Fatma Salum (MAELEZO)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hivi ni lini tutakuwa na aibu jamani? Shule zinafungwa kwa sababu hakuna chakula, wewe uliyekalisha makalio yako daresalam unaviambia vyombo vya habari kuseme zimefungwa kimakosa kwani chakula kipo. What the F...K (nimesahau kwamba luka hawezi kupost mpaka ubalozi wake umkubalie huko dc.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...