Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

TANZANIA inatarajia kushiriki maonyesho ya nchi 149 ya bidhaa za  viungo ambapo watanzania 500 wanatakiwa kushiriki maonyesho hayo yanayotarajia kuanza Mei 1 hadi 31 mwaka huu mjini Milan Italia.

Akizungumza na waandishi habari ofisini kwake katika  viwanja vya Mamlaka ya Maendeleo ya Tanzania(Tantrade),Jacqueline Maleko,amesema maonyesho hayo ni fursa ya watanzania kujifunza mbinu mbalimbali za kutanua wigo wa biashara.

Jacqueline amesema kuwa Tantrade imefanya mawasiliano na katika sehemu ya maradhi pamoja na mashirika ya ndege kwa kwa siku tano ambayo itagharimu dola za Kimarekani 1500,hivyo watu mbalimbali wameombwa ili kuweza kusogea mbele kiuchumi kutokana na elimu watakayoipta katika maonyesho hayo.

Amesema maonyesho haya yatalenga katika sekta ya chakula pamoja na teknolojia mbalimbali duniani zitaendeshwa kwa kauli mbiu ya ,Kulisha Dunia Nguvu ya Uhai. 

“Hatuwezi  kukua kiuchumi katika biashara za nje kwa kukaa ndani bila kuweza kupata mawazo kutoka kwa nchi zilizo endelea kiuchumi katika nyanja za maendeleo kutokana na biashara za nje”amesema Jacqueline.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa Biashara za Nje,Anna Bulondo,amesema maonyesho ya biashara ya mwaka huu yatakuwa ya aina yake kutokana na mbaoresho mbalimbali na 24 hadi sasa zimedhibisha kushiriki maonyesho hayo.

Amesema katika mwaka huu watatoa tuzo kwa banda bora hivyo wanatakiwa kufanya maresho ya mabanda hayo ili kuweza kupata tuzo hiyo. Viingilio katika maonyesho ya 39 ya biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam vitakuwa sh.3000 kwa wakubwa na watoto Sh.1000.
  Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE (katikati) akizungumza katika mkutano wa maandalizi ya maonyesho ya 39 ya kimataifa  ulifanyika katika viwanja vya SabaSaba jijini Dar es Salaam leo.
 Mkurugenzi wa Biashara za Nje,Anna Bulondo, akizungumza katika mkutano wa maandalizi ya maonyesho ya 39 ya kimataifa  ulifanyika katika viwanja vya SabaSaba jijini Dar es Salaam leo.
 Baadhi ya wandishi wa habari waliohudhurika katika mkutano wa maonyesho ya 39 ya biashara ya kimataifa,ulifanyika katika viwanja vya Saba Saba jijini Dar es Salaam leo. (PICHA NA EMMANUEL MASSAKA,GLOBU YA JAMII).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...