Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa
Mlipa Kodi Kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo
akitoa neno kuwakaribisha wageni katika mkutano wa Kwanza wa Wakuu wa
Vyuo vya Kodi Afrika uliohudhuriwa na wajumbe zaidi ya 50 kutoka katika
taasisi za kodi barani Afrika, Mkutano huo umeandaliwa kwa ushirikiano
wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Taasisi za Kodi Afrika (ATAF), Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Kodi
Tanzani (ITA) Prof. Isaiah Jairo akiongea na wajumbe wa mkutano huo na
kueleza namna utakavyosaidia katika kuzijengea uwezo Taasisi za
ukusanyaji kodi Afrika hivyo kuweza kuinua uchumi wa Mataifa mengi ya
Afrika.
Mkurugenzi wa Ujengaji Uwezo
kutoka Taasisi za Kodi Afrika (ATAF) Bw. Kennedy Onyonyi akiwaeleza
wajumbe wa Mkutano huo namna Kamati hiyo inavyoshirikiana na Taasisi za
Kodi Afrika katika kuzijengea Taasisi hizo uwezo wa Kiutendaji na
kusaidia nchi wanachama kushiriki kuwa na sera ya pamoja ya masuala ya
Kodi ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji kodi.
Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA) Bw. Lusekelo Mwaseba Akiongea na wajumbe
waliohudhuria Mkutano huo namna Tanzania ilivyofurahishwa na kuwa
mwenyeji wa Mkutano huo wa Kwanza wa wakuu wa vyuo vya uongozi wa Kodi
Afrika na kuwataka wajumbe kutumia fursa hiyo kujifunza masuala
mbalimbali katika sekta hiyo ya ukusanyaji kodi kwani ni moja ya mhimili
muhimu wa maendeleo kwa Mataifa mengi duniani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...