Mwenyekiti wa Chama wafanyakazi wa sekta ya usafirishaji
,Sharifu Mohamed akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salam juu ya wafanyakazi wa sekta hiyo kutojihusisha na migomo ,Kuhoto  Katibu Mkuu  Salum Abdallaha TAROWU,kulia Mlezi wa TAROWU,Yakuub Rajabu (Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii)

Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

CHAMA cha  wafanyakazi wa usafirishaji kwa njia ya barabara Tanzania (TAROWU)  kimewatahadharisha  wafanyakazi wa sekta ya usafirishaji  kutojihusisha na mgomo katika sekta ya usafirishaji.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Chama hicho,Sharifu Mohamed amesema wafanyakazi wa sekta ya usafirishaji wakijihusisha katika migomo watasababisha kushuka kwa uchumi kutokana na sekta hiyo ilivyokuwa muhimu. 

Mohamed amesema serikali inatakiwa kuchukua maamuzi magumu kwa wale ambao watahusika na migomo ambayo inalenga kupoteza haki za wafanyakazi katika sekta hiyo.

Amesema madai yanayotolewa na wafanyakazi wa sekta ya usafirishaji kuwa serikali imeweka sheria ya kuwatoza madereva sh.550,000 hayana ukweli wowote ni viongozi kutaka kuhalalisha mgomo huo.

Mohamed amesema waajiri wanatakiwa kuwalipia gharama za mafunzo kwa madereva wao ili waweze kufanya kazi hiyo kwa ufanisi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...