
Mtaalamu wa mawasiliano Mradi wa uwezeshaji wa demokrasia (DEP) kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Nicodemus Marcus akizungumza wakati wa kufunga warsha ya siku tatu ya kutathmini mradi wa uwezeshaji wa demokrasia na amani (DEP) kwa wanamtandao wa Redio Jamii nchini (COMNETA) yenye lengo la kuimarisha ushiriki wa redio za jamii nchini kuelekea uchaguzi 2015 na kura ya maoni iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na kufadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria Tanzania jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wa pili kushoto ni Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu,akifuatiwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania, Prof. Tolly Mbwete, Mwenyekiti wa mtandao wa Redio Jamii nchini (COMNETA) ambaye pia ni Mkurugenzi wa Redio ya Jamii ya Wilayani Karagwe ya FADECO FM, Bw.Joseph Sekiku na Mshauri wa UNESCO, Balozi mstaafu Mh. Christopher Liundi.
Na Mwandishi wetu
SHIRIKA la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini limetoa wito kwa redio za jamii kujikita zaidi katika kutoa hamasa ya ushiriki wa wananchi katika mchakato wa uchaguzi ukiwamo kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Akizungumza matumaini ya Umoja huo katika tathmini ya mradi wa Uwezeshaji wa Demokrasia (DEP) kwa Redio za Kijamii nchini Tanzania zinazounda umoja wa COMNETA, chini ya ufadhili wa UNESCO, mtaalamu wa masuala ya mawasiliano wa UNDP Nicodemus Marcus alisema kwamba redio hizo zina kazi 5 muhimu kuelekea uchaguzi.
Alisema pamoja na kutekeleza makubaliano kati ya Umoja wa Mataifa na redio hizo kuhusu elimu kuelekea uchaguzi mkuu unaozingatia maadili ya uandishi na uwajibikaji katika mradi huo ni matumaini ya UNDP kwamba redio hizo zitatimiza wajibu wa kuhakikisha kwamba uchaguzi unafanyika kwa amani na makundi mbalimbali yanajitokeza kupitia vyama vyao vya kisiasa kuwania uongozi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...