Mkuu wa Oganaizesheni wa NCCR-Mageuzi,Faustine Sungura akizungumza na Wandishi wa habari katika Makao Makuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi,leo jijini Dar es Salaam,(kushoto) ni Katibu wa Vijana wa  Chama cha NCCR-Mageuzi Taifa Mawazo Atanas.
 Mkuu wa Oganaizesheni wa NCCR-Mageuzi, Faustine Sungura akimkabidhi fomu ya kugombea nafasi ya Urais Katibu wa vijana wa  chama cha NCCR-Mageuzi taifa Mawazo Atanas kwa niaba ya  Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,Dk George Mihango,jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano wa kumkabidhi fomu ya kugombea nafasi ya urais Katibu wa Vijana wa  Chama cha NCCR-Mageuzi Taifa,Mawazo Atanas kwa niaba ya Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,Dk.George Mihango,leo jijini Dar es Salaam. (Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii)

Na  Avila Kakingo,Globu ya Jamii
UMOJA wa Vijana wa Chama cha NCCR-Mageuzi  wamemchukulia fomu ya kugombea nafasi ya Urais kwa chama hicho,Dk.George Mihango ambaye ni Mhadhiri wa  Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya Chama hicho, leo jijini Dar es Salaam,Mkuu wa Oganaizesheni wa NCCR-Mageuzi, Faustine Sungura,amesema vijana wa chama hicho wamemshawishi Mhadhiri huyo kwakuwa anavigezo vyote vya kugombea nafasi hiyo.

Sungura,amesema kuwa milango iko wazi kwa wanachama kuja kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali katika chama hicho katika uchaguzi unaotarajia kufanyika hivi karibuni.

Aidha amesema,wakati umefika kwa  vijana waliozaliwa baada ya uhuru sasa wanaweza kugombea nafasi za uongozi katika  chama hicho, kutokana na uwezo wanaonyesha katika vitu mbalimbali.


Nae Katibu wa Vijana wa  Chama cha NCCR- Mageuzi Taifa,Mawazo Atanas amewashukuru vijana wa chama hicho kwa kusaidia kumchagua Mhadhiri wa Chuo Kikuu  cha Dar es Salaam,Dk.George Mihango kuchukua fomu kwaajili ya kugombea nafasi ya Urais katika chama hicho ambaye atachuana na wagombea mbalimbali katika nafasi hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...